Thursday, November 12, 2009
ndoa na kushirikishana.
kwa hiyo katika ndoa jambo la msingi ni kushirikishana. ukimshirikisha mwenzio, ni ishara nzuuri sana ya kumjali, kumpenda na kumheshimu. ukimshirikisha mwezio ataona ni kwa kiasi gani yeye ana umuhimu kwako. tushirikishane hata vitu vile vinavyoonekana ni vidogo na kumbuka hamna vidogo balli hata vile vikubwa, huanza vikiwa vidogo pia.
tatizo la kushirikishana kwetu huwa siko kule kwema zaidi. mnatoka kazini na kuleta changamoto zoote huko nyumbani na hakuna kuongea wala nini. harafu usiku wa manane mtu anashangaa ghafla huyoo uko kifuani, unataka kumshirikisha tendo la ngono! wapi na wapi, huko kutakuwa ni kubakana na sio kushirikishana wala nini.
ni lazima tuwe na wakati wa kuongea na wenzetu, kuwaomba ushauri. kila ngazi ya maisha yetu, ni lazima tuelezani nini kinaendelea badala ya siri. kushirikiana kuna faida nyingi sana na ni mbolea ya familia au mahusiano yetu. na sio kushirikiana tu bali pia kubebeana mizigo
Wednesday, November 11, 2009
toooo busy jamani
Tuesday, November 10, 2009
Saturday, November 7, 2009
Tunaendelea na ndoa.
Tulipotegemea raha tunaanza kutatizwa. Na badala ya kusimama kwenye nafasi zetu, tunakaa pembeni na kuwaita wengine ili waje kumaliza matatizo yetu utadhani ni yao na wao wakija kazi kubwa ni kusimamia upande wao na kuuponda mwingine kwamba kama ulienda kwa ndugu wa Mume, basi watavutia upande wao na wakike hivyo hivyo. Hata hivyo tuyaitayo matatizo sio matatizo bali ni changamoto tu
Kwa mfano; baba yangu alioa wake wawili kwa nyakati tofauti na hakuweza kuisha na mke hata mmoja. Baba alimwoa mama wa kambo au mke wake wa kwanza na kuzaa naye watoto watatu, baadaye mambo hayakwenda sawa, wakafukuzana na kumwoa mama ambaye pia niliambiwa kuwa walifukuzana nikiwabado mtoto mdogo na wa mwisho nikiwa nina siku chache hapa duniani kama mwaka au pungufu.
Nilijaribu kufuatilia kilichompelekea baba kushindwa kuisha na mama au mama wa kambo na kwa bahati mbaya baba aliisha kufa na hivyo sikuweza kusikua hilo kutoka kwake. Nikiwa nimelelewa katika familia ya upande wa baba niliweza kumsikia mama yake baba (bibi yangu) akiwalalamikia wale wake zake baba kuwa walikuwa watu wa ajabu wasiofaa kuolewa na baba. Mashangazi pia walilalamika, unashindwa kujua nani alioa baba, bibi au nduguze?
Pamoja na kwamba mama alitoka kijiji jirani sana na pale nyumbani, sikuwahi kuambiwa kuwa kuna mama na kuna shangazi niliyedhani ndiye mama. Nilipokuwa mkubwa na kuanza kuongea na watu wa nje, ndo nikaaza kuambiwa habari za mama yangu. Baadhi ya watu walilia machozi kuona simfahamu mama na nduguze
Daima bibi na mashangazi zangu walinisimulia ubaya wa wake za baba akiwemo mama utadhani sio mama yangu na waliniambia mpaka matusi makubwa na sijui lengo nini na nikijaribu kuamini kuwa labda mama ni mbaya japo alinizaa. Niliona kasoro moja ambayo ilikuwa ni kunizuia kumwona mama au nduguze na nikajiuliza ni kwanini wasiache nijionee huo ubaya??
Kama mtoto nilikuwa ‘victim’ wa maamuzi yao kiasi kwamba nilikuwa najiuliza mama ni yupi kati ya wanawake wote niliokuwa nakutana nao njiani. Ukafika wakati nikaweza kumwona mama wa kambo na baadaye mama. Wote kwa pamoja waliwalalamikia bibi na mashangazi zangu (mawafi) juu ya ndoa na sio baba! Nikashangaa.
Nikienda huku naambiwa hivi na huku hivi. Bahati mbaya baba alikwisha kufa ila nikashangaa wake zake baba wanawalalamikia mawifi na mama mkwe na sio mume. Nikajumuisha maongezi na kugundua tatizo kwamba baba aliwaamini sana nduguze na kuwaeleza kila kitu na kuwaomba wasaidie kusulushisha au aliacha maisha yake binafsi na ndoa yake mikononi mwa watu wengine
Hilo ni sehemu ya tatizo la ndoa. Kutokuwa sisi na kuona changamoto kama matatizo makubwa na kuwaomba wengine waje kusuruhisha. Kufanya hivyo ni kuigawa ndoa na kujiletea matatizo kwani katika jamii zetu hizi za kiafrika au kama binadamu wenye uhai, ni lazima kutakuwepo upendeleo na ubaguzi wa kumwona auliyenaye kuwa ni mtu mbaya kwani sio ndugu yako.
Hii ni hatari na wanawake ndio waathirika wakuu. Inafika hatua mwanandoa wako haonekani kama mtu na wewe unamdharau kwa ubadguzi na kuona mabaya yake kuliko mazuri utadhani unaweza kuishi na ndugu zako wakawa kama yeye. Hii ni hatari sana kwa ndoa.
Upatapo matatizo katika ndoa, jambo la kwanza ni kwa kusuruhisha na mwanandoa mwenzio. Jinsi ya kusuruhisha ni kukaa kwa muda na kuongelea tatizo kwa kusikiliza kwa makini. Ikiwezekana mwondoke nyumbani na kwenda mahala patulivu na kuongea vizuri.
Msipoelewana basi tafuta mshauri. Mshauri awe ni yule unayemwamini na asiyekuwa na upendeleo, atakayewasikiliza na kutunza siri, ni vyema asiwe na uhusiano (hasa wa damu) na familia ya mke au mume. Ndugu zako na wazazi wako (wa mke/mume) wanaouhuru wa kutoa maoni lakini usiwape sana nafasi kwani wanaweza kuja na upendeleo au hata wivu.
Matatizo ya kindoa huathiri zaidi watoto wasiohusika kama mimi nilivyoathiriwa kiasi chake. Lakini uhai wa ndoa umo ndani mwako.
Ni hayo kwa leo, barikiwa na mjadala unaendelea
Wednesday, November 4, 2009
tuoavyo na tuishivyo katika ndoa
katika mada iliyotangulia juu ya ndoa tumeona maoni kadhaa juu ya ndoa na sababu za kuoa. wengi wamesema mazuri ila sijaona aliyesema kuwa ndoa ni tendo la ndoa na hivyo kuhalalisha msimamo wangu kuwa sio tendo la ndoa bali tendo la ngono kwani kulifanya sio lazima uwe kwenye ndoa au kulifanya pia sio lazima lilete mimba na kuzalisha mtoto kama baadhi wasemavyo ni tendo la kuzaa watoto.
basi sababu za kuoa na jinsi ya kuoa na nani tuoane naye huwa sio zetu na labda hili ndilo tatizo. mara nyingi 'tunalazimika' kuoa kwa vigezo vya umri, kampani nk na wengine hulazimishwa na wazazi, ndugu au jamaa lakini kuna wanaolazimishwa na dini au kwa kuwa alimpa mimba bila kujua kwani alitaka ngono tu ya maa moja, basi kalazimika/mishwa kumwoa au kuolewa naye!!! wengine ni mali au fedha alizonazo yule amtakaye na mwingine ni uzuri wa huyo! wengi sasa hatufanyi ndoa zetu kwa maaamuzi yetu na mapenzi yetu bali ya wale wanaotuangalia utadhani wanatusaidia kuishi au wanaoa wao.
hivyo basi, kwanza tunataka tuolewa na mtu mwenye nazo au ambaye watakukoma naye wakikuona naye, kwa hiyo tunatanguliza ya nje yetu kuliko ya ndani mwetu. hata hivyo ukiongea na walioko kwenye 'ndoano' zitokanazo na ndoa, watakwambia kuwa walidhani watapata furaha au ndo mwenzi wa maisha. ndoa nyingi za matajiri na masikini ziko kwenye hati hati na upendo hakuna. majamaa hayaelewani tena.
kuingia kwenye ndoa ukitarajia kupata furaha ni ajabu kwani furaha ya kweli haipo kwenye ndoa bali imo ndani mwetu na kama hatuwezi kuigundua hiyo, ni vigumu sana kuipokea kutoka nje yetu (kwa wengine) na hivyo hubakia kuwa wa masikitiko na vilio na kusaga meno. kwa kujua furaha hiyo na kuishea na wengine ndipo itakapo kuwa na manufaa badala ya kuitegemea kutoka kwa hao tuoanaonao.
tukiisha kuingia kwenye ndoa tunapenda jamaa watuone tulivyo kuwa na vifaa vikali na nini sijui. lakini wakati mwingine tunadhani tuliwatafuta wenza kumbe tulikutanishwa nao tu kwa sababu ya nguvu za maumbile kutokana na maneno yetu, matendno yetu na maisha yetu ya sasa au yaliyopita.
kwa leo ni hayo tu na next ijayo tutaona juu ya maisha yenu wawili baada ya kuwa mmeoana na hapo ni muhimu kwani kumbuka wale waliokusurutisha uoe au wale uliotaka kuwatambia kwa bonge la harusi hawapo tena au uliowaolea kimwana mkali sasa wanamkonyeza na kutaka kunyatia.
ni nyakatii pia ambazo kama ulipenda ngono basi uezoea na kuiona sio dili tena au unawaona wengie wazuuri nje. au ni wakati ambao sasa mimba zinakuja au zinagoma na kumbuka hukujiandalia lolote kwani maisha yako yoote ulikuwa ukiiwazia siku yako ya kufunga ndoa na sio maisha yako na mwenzako. C U
Monday, November 2, 2009
Maisha ya ndoa na ndoa yenyewe.
Hivi ni kwanini watu wanaoana? Ni swali gumu. Wengi watakwambia wanatarajia kupata furaha,amani, upendo na ridhiko kutoka kwa wamuoaye, wengine watasema umri wa kuoa umefika na wengine watasingizia dini kuwa Mungu aliagiza kuwa tuoane.
Hata hivyo karibia 90% ya ndoa hazina amani, hazina upendo wala ridhiko na hazifai na zimebakia kuwa ndoano. Ni kamba au mnyororo wa kuwafunga na kuwalazimisha na kuwavutilia matatizoni.
Blog hii sasa imeamua kuanza kujadili juu ya ndoa. Huko Nyuma tulijadili juu ya tendo la ngono (wengine waliliita tendo la ndoa) na kujikuta kuwa tumesahau swala muhimu ambalo ni ndoa. Ukimuuliza mtu aliyejitambua kuwa ni kwanini kaoa au olewa atakwambia kuwa ni kwa sababu labda ya kupenda ngono au kampani au kuzaa au nini sijui na nakumbuka nilipomuuliza yule wangu aliniambia kuwa anapenda hicho kitamu zaidi.
Kwa nini ndoa ni ngumu na nini kifanyike ili zisiwe ngumu, ziwe nzuri, tamu na nyepesi? Waliojitoa kwenye ndoa na kuamua kwenda nje ya ndoa wamekuta kuwa hawawezi, walio waacha wenzi wao na kuwaoa wengine, wamekuta ubaya kuliko walikotoka na ni bora warudi kule.
Sasa ishu iko wapi na ninini kifanyike?
Saturday, October 31, 2009
I love the children
Thursday, October 29, 2009
Tuesday, October 27, 2009
Ziara ya kanda ya ziwa imekwisha
mikoa ya shinyanga, kagera, mara na Mwanza, mambo ni mazuri muno kiasi kwamba naiga story ya kwenye biblia kuwa nikae huku huku yaani nijenge vibanda na ikizingatiwa kuwa nimeishamalizia muda wa kuishi Dar
Musoma kila mtu ni mbabe na inabidi uwe makini kwani ni wataalamu wa kurusha mawe kuliko risasi. mwanza ni jiji mchanganyiko lililozungukwa na migodi yote mikubwa ya nchi hii wakati Bukoba mvua zinanyesha ni matoke kwa wingi na mikogo ya kinshomile bado inashamiri.
wewe. natuone uchaguzi mkuu ujao si wa mitaa umetuonyesha muelekeo???
see yu in dar soon
Sunday, October 25, 2009
Yasinta wa ruhuwiko na asiyefunzwa na mamaye.........

!!!!
Yasinta pichani anasema.................
........asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu nami nikamuuliza kama mamaye huyo anaishi wapi? si iulimwenguni humo humo na hakuna tofauti kati ya mafunzo ya mama na ulimwnegu kwa sababu wote ni wamoja yaani wa ulimwenguni?
basi nimemaliza ziara yangu kwa wanyanchoka na hawana lolote kumbe mapigano yao ni ya kizamaani tu na nimetoka nila hata kipande cha ngewe ila duh mambo ya hapa!!!!
Friday, October 23, 2009
MISOSI YA BUKOBA EMAIL KUTOKA KWA MWANAKIWE WA BUKOBA

HII NDIYO BUKOBA YENYE NEEMA.
Kwa miaka kadhaa sasa nimekuwa mkazi wa mji wa Bukoba Kata ya Hamugembe, Mtaa wa Omukishenye(eneo lenye mchanga). Nimeanza kuishi Bukoba bila ajira wakati huo nilikuwa nachukua kozi ya Hotel Management na kwa bahati mbaya shule hiyo haikuwa nabweni hivyo tulilazimika kuishi street na kujitegemea wenyewe. Niliemea chakula, mkaa namahitaji mengine then nikawa nawajibika kuandaa mwenyewe.
Ninachotaka kuongelea ni maisha ya Bukoba yalivyo cheap kwa upande wa chakula ukilinganisha na miji mingine size ya Bk. Kwa Bk chakula kikuu huwa ni Ndizi (Ebitoke), na hii ni kwa makabila yote yanayoishi Bukoba asijeakakudanganya mtu eti ni chakula maalumu kwa wahaya tu, HAPANA.
Simnajua kuwa chakula kikisha kuwa na unafuu mambo yote yana…. Kama unavyoona picha za magari yenye chakula , hiyo mizigo wala haiendi soko kuu ila inaenda kwenye ka soko kadogo ka mtaa wa Omukishenye. Ndani ya ka soko hako huwa yanaingizwa magari yaliyosheheni kama unayoyaona pichani manne kwa siku za Jumanne na Ijumaa(Hizo ni shehena za ndizi, kabeji, palachichi, nanasi , nyanya, nyanya chungu , mihogo, magimbi pamoja na mengine kibao. Pamoja na shehena hiyo kuingia mtaani kwetu sasa neema unakutana nayo katika bei. mie huwa najisikia kumpa sifa Mungu hasa nikiona unapata mfungu wa magimbi kwa shilingi mia tano tu. Mimi sina familia kwa hiyo huwa sijishughulishi na mambo ya kupika, ila nilibahatika kuonea na rafiki yangu mwenye familia(mme, mke, mfanyakazi na mtoto) yeye aliniambia magimbi ya shilingi mia tano tu ni mlo tosha kwa familia yake tena wakati mwingine kunakuwa na ziada, na vyakula vingine kama mihogo na ndizi hali inakuwa ni hiyohiyo. Kwa nanasi huwa ni shilingi 200 – 500.Mji wa Bk huwa unategemea sana kupata vyakula kutoka Wilaya za Muleba, Bkb vijijini-IZIMBYA na Karagwe kwa % kubwa. Hapa nimeongelea tu kwa mtaa wa Omukishenye lakini panapo majaliwa nitakuonyesheni hata Soko kuu ili uone mwenyewe.
Mungu ibariki Bukoba
mapenzi ya enzi na enzi
nilapo chakula nakuona kwenye beseni na kila nikioga nakuona kwenye bakuli.
wewe ndiye wangu kwa kweli nakupenda kuliko hata wazazi na sasa sijui nifanyeje kwa kukupenda ila tu jua ya kwamba nitakupenda mpaka basi"
duh!!!!!
Wednesday, October 21, 2009
Bukoba ni mvua za kufa mtu
mikoa yoote ya nchi hii imekauka, ni ukame na ninjaa lakini mkoa wa kagera mvua zinanyesha na mazao yanaendelea kukua shambani na yanayovunwa basi huuzwa nchi jirani ya Uganda wakati mikoa iliyobaki ikiwa na njaa za kutosha na vyakula bei juu.
inashangaza ni kwa nini vyakula vielekee uganda na sio mikoa baki ya tanzania. labda ishu ni bara bara na njia za usafirishaji kwani ni rahisi saana kusafirisha bidhaa yoyote kuelekea uganda kuliko Tanzania
anyway haka ni kanchi ka ahadi ndio maana vyakula na mvua vya kufa mtu na labda ni hamie huku bongo
napiga hodi kwa Wanyanchoka na wanyanchori eti naenda kuwapiga utambuzi wakati wana mishale, mikuki na ni wataalamu wa kurusha mawe wakila Nyama na kunywa damu mbichi inayowatia unyama. je nitaweza kuwapatia utambuzi bila kula jiwe? mkiona kimya mjue washanitenda wale.
najiamini
Tuesday, October 20, 2009
Monday, October 19, 2009
nimepokea barua juu ya uchafuzi wa mto kanoni
Pole na majukumu, nimetuma ujumbe huu nikijua kuwa uko bush ila ukija mjini tu utaupata.
Kila ninapo jaribu kutoa comments zangu kwenye mada zako nashindwa, labda ni kwa vile hii technology kwangu haijapanda, but i hope utanielekeza vizuri tu pindi tukionana au waweza kunielekeza hata kwa njia ya maandishi.
Maoni naweza kutoa au nisitoe kitu cha muhimu kwangu ni kupata muda wa kusoma zile mada zako na kuzitafakari.
Bila shaka wewe ni mtu unayeifahamu vizuri Bukoba, hapa huwa kuna ka mto kanoni kale ambako kanamwaga maji yake ziwa V. Mimi huwa nakapenda kwa jinsi kalivyo kaakaa ila nimekuja kusikitishwa na kitu kimoja kinachoitwa uchafuzi wa mazingira/kanoni. kitu ambacho sikukielewa ni pale tu maeneo ya Hamgembe inayopakana na Migera lakini inatenganishwa na mto kanoni kuna vituo zaidi ya 10 ambavyo vinaendesha shughuri za kibinadamu. Mfano: kufua, kuosha vyombo, kuosha pikipiki, kuoga na mengine mengi ambayo kwa kweli yanatia kinyaa hata wewe ukiona.
Hivi kweli najiuliza kwa staili hii tutawezaje kutunza mazingira? nimebahatika kupiga picha moja ya shughuli zilizo kuwa zikiendeshwa pale, KWA KUJIFICHA LAKINI
Sunday, October 18, 2009
mtandao unagoma kidogo.
aminia
Thursday, October 15, 2009
nimejifunza mengi kule bushi kwetu
nilienda kupumzika na sikuenda kutembea tembea lakini nilikutana na mzee mmoja mwalimu mstaafu maarufu kama mwl Mushumbusi ladislausi, ni mkatoliki mzuuuri ambaye kaamua kumpeleka mwanae wa mwisho Lwejuna almachius kusomea taaluma ya kutoa kibubusa (dogma) namaanisha uongozi wa kuchunga kondoo wanaosimama kwa miguu miwili, namaanisha watu na hivyo kaenda kusomea upadre
basi aliniambia kuwa kijana wake anasomea falsafa. akaanza kuniambia juu ya umuhimu wa kusomea falsafa na kwamba ni somo muhimu kwetu kama kweli tunataka mambo yanyooke vizuri kwetu katika ngazi za kijamii na hasa 'si-hasa' namaanisha politiks
mzee Mushuimbusi anasema wanasiasa woote makini wanaojenga hoja na kutetea maslahi ya wengi wamesoma falsafa. anasema Nyerere ni mwanafalsafa, Slaa, Zito Kabwe na wengineo. je ni kweli tunahitaji wanasiasa wa kifalsafa-falsafa kama anavyodai ndg Mushumbusi? je we mtizamo wako ni upi? kuna ushahidi mwingine juu ya hili?
kitururu je?
Friday, October 9, 2009
kupotea kijiweni kwa siku kadhaa


wanakijiwe, baada ya kufika mjini bukoba na nikiendelea vyema na maandalizi ya kutoa mada za yutambuzi mjini hapa, naomba radhi kwamba sitakuwepo kijiweni hapa kwani naingia msituni kidogo kama zinavyoonyesha picha hapo juu.
ni miaka mingi sana sijafarrahia maisha ya kijijini lakini hata hivyo nimeamua kwenda bush wenyewe wanaseama kusafisha nyota. naenda kukaa migombani na ku-meditate kwa muda mrefu huku nikikaa na wazee wangu na washikaji wakule kwa muda usiojulikana lakini sio mrefu sana. nitaoga mtoni na nitazima mawasialiano yoote ili niipata fresh kule
kwakuwa mimi ndiye mtundika mada kijiweni hapa, msishangae mkiona kimya jamani. nitawaletea habari mpya kwani nitatoka huko nikiwa kiumbe kipya kabisa.
all the best na furahieni maisha.
Thursday, October 8, 2009
nimetua mjini Bukoba jamani.
Monday, October 5, 2009
maisha yetu na... makala katika kwanza jamii
Maisha yetu ni yale yale ya kukimbizana na kukimbilia kilicho mbali siku zote. Tunatamani mishahara mikubwa, vyeo vikubwa, wenza wa aina fulani fulani. Tunatamani na kuishi kwa utashi zaidi wala sio kwa mapenzi ya kweli na uhalisia kiasi kwamba dunia inatisha sisi siku zote tunaogopa tu.
Ukiwa na waliokuzunguka, hamkosi kutofautiana, ukiwa peke yako, ndani mwako kuna kelele na vurugu nyingi. Unatamani kufungulia redio, kusoma kitabu, gazeti au hata msaafu. Au unatoka ili utembeetembee nakadhalika.
Sasa maisha yanaaza kukutishia. Ni magumu, huwezi kukaa peke yako, unatamani uwe na wengine, ukiwa nao, hamkawii kukosana na kugombana. Na hii ndio sababu familia nyingi zina migogoro. Tunaona makosa kiurahisi kuliko mazuri au hata kusahihishana. Maisha ni ya masharti kweli kweli.
Tunatafuta mali na kujitahidi kumiliki mali nyingi zaidi ili tuumiliki ulimwengu na kuna wanaojiaminisha kuwa wanamiliki ulimwengu kumbe ni mateso matupu. Unafikiri marais na wabunge na wengi wa wennye utajiri mkubwa wana amani yoyote na kuona maana halisi ya maisha? Hawana. Wanatawaliwa na hofu, huzuni ni kuhangaika ili waendelee kuwa madarakani na sio kutumika wala kutumikia kama inavyopaswa.
Tunakufa kwa presha kwa sababu ya kutaka kumiliki kitu fulani na tunasahau kwamba kuna kitu muhimu tunachokimiliki ambacho ndicho cha kujivuna nacho kuliko vinginevyovyote viwavyo. Kitu hicho ni sisi wenyewe. Hakuna awezaye kutumiliki sisi isipokuwa sisi wenyewe tunajimiliki. Badala yake tunakimbizana na vile vya nje yetu tukidhani vitatupa furaha kumbe furaha ya kweli imo ndani mwetu.
Nilikutana na binti mmoja ambaye ni mhitimu wa chuo kikuu cha Dar es salaam. Binti huyo aliniambia kuwa anafanya kazi fulani ya kuingiza takwimu katika tarakishi. Nilimpongeza na kumtakia mema lakini yeye hakutaka na wala hataki hayo mema niliyomtakia kwani alinieleza kuwa akipata kazi kwingine anawezakuachana na kazi ile kwa sababu eti haimuhakikishia ¨future¨ au maisha ya baadaye
maisha ya baadaye maanake nini nini? Anafikiri mshahala anaolipwa hautoshi. Anatamani mshahala zaidi. Ndivyo ilivyo katika maisha ya jamii yetu na kwa walio wengi. Hatufanyi kazi kwa bidii wala kwa malengo fulani, bali tunatafuta vyeo, tunatamani pesa zaidi ya tunazolipwa sasa na tunatamani kumiliki mali nyingi zaidi ya tulizonazo sasa.
Katika ofisi za umma kwa mfano, naibu katibu mkuu anatamani kuwa naibu waziri, huku katibu mkuu akitamani kuwa waziri na waziri anatamani kuwa waziri mkuu au rais. Ndivyo ilivyo, na rais anatumia kila mbinu kuhakikisha anaedelea kuwa rais na furaha ni kwamba hapa Tanzania hatujapata rais wa kubadili katiba ili afie madarakani kama zilivyo nchi nyingine kama Uganda , Libya au Zimbabwe .
Tamaa za vyeo na mali ndizo zinazotuzuia kuishi kwa malengo na badala yake tunatamani nakuamua kuwa mafisadi. Tunaipenda na kuitumikia miili yetu utadhani haitakuja siku tulazimike kuiacha (kufa). Tamaa hizo ndizo zinazotupeleaka jela, kuishi kwa hofu, wasi wasi na mamjuto.
Mmoja kati ya maafisa wa benki kuu walioko rumande kwa tuhuma za ufisadi, ni mkristo mzuri na mzee wa kanisa mojawapo la KKKT jijini Dar esalaam. Wazee kama huyo ndio walioko mstari wambele katika mambo ya kanisa. Wanaonekana kumjua Mungu kuliko wengine na sasa maandiko ya biblia yanaanza kuwageuka kama lile lisemalo yaliyofanyiwa gizani yataanikwa nuruni. Ulokole wao sasa wanatamani kuukana hukuwaumini wenzao waliobaki nyuma wakijaribu kuwaombea kwa Mungu asiyekuwa fisadi. Kwa nini wanawaombea? Labda hawawaombei wale walioko rumande, wanajiombea kwani wanajua kesho yaweza kuwa wao.
Tunajitengezea wenyewe jamii ya vurugu iliyojaa visa na visasasi, yenye kushitakiana na kukwaruzana. Hatujikagui ndani mwetu, tunalalamika tu muda wote na kuwalaumu wengine. Ikifika zamu yetu tunaona kama tunaonewa. Kumbe wale tunaowalaumu sio wao bali tunaona ishara ya mabaya yetu kupitia wao. Tunakila haja ya kujitambua na kujua nafasi yetu katika jamii badala ya kuishi kwa tamaa na kuongozwa na hisia.
Sisi kama binadamu ni lazima tujue kazi iliyotuleata duniani na kuitumikia vyema badala ya kutanga tanga. Matatizo yanayoikumba jamii yetu kwa kiasi kikubwa ni kwasababu wengi wetu hatuajaamua kuisaidia jamii na badala yake tumekamatwa na tamaa ya kutoridhika tukabakia kuwa wa kukimbiza kilicho mbali yetu na kugáng´ania tulicho nacho. Sio wa kutumia tulichokwisha kuwa nacho na badala yake tumeendelea kufukuza cha mbali na kulimbikiza hata tusichokihitaji.
Tunashindwa kujua kuwa kila kitu ipo siku tutakiacha. Dini zetu nazo zinasisitiza waumini wake kukusanya pesa nyingi kwa njia za matoleo mbali mbali badala ya kuwakuza kiroho kama kazi kuu na ya msingi ya dini hizi na labda ndio sababu mafisadi wanakumbatiwa katika nyumba za ibada kuliko wasiokuwa mafisadi ambao hawana pesa nyingi za kutoa na labda tusema masikini.
Masha yetu yameedelea kuwa ya kujisifia jinsi tulivyosoma, tunavyojua lugha za kigeni, tunavyokula vyakula vizuri, ulevi na hata umaarufu. Vyombo vyetu vya habari vimejaa habari za kushtusha pekee na kutishiana utadhani hamna mambo muhimu ya kuelimisha wananchi. Vimekuwa ni vya kuandika na kutangaza habari zisizonamuhimu eti kwa sababu tu zinalipa.
Tunahitaji jamii bora. Jamii inayoishi kwa malengo, jamii iliyojitambua. Tusipoweza kupunguza tamaa, wakati utafika na sasa upo karibu ambapo ufisadi na vitendo viovu vitageuzwa kuwa halali. Bila kujitambua na kuishi kwa uhalisia, maisha yetu yatakuwa ni kazi bure. Kipi muhimu kati ya kuishi kwa mshikamano,umoja utu, kufanya kazi kwa bidii kwa faida ya wengi na kuishi kwa ubinafsi, uchoyo na tamaa?
Si kila mtu alikufa au atakufa? Kipi bora kati ya kujilimbikizia mali ili uishi kwa wasi wasi, hofu au kuwa mlinzi wa mali hizo na kuishi maisha mema yenye malengo na nia za kweli? Kwa nini tunasoma? Ili tutagatange tukitafuta mali zaidi mpaka tuishie kuwa wezi, mafisadi na matapeli au tuisaidie jamii yetu hata sisi wenyewe kwa kula jasho letu na halali yetu?
Kwa nini tusiishi kwa upendo na kueneza upendo? Kwa nini tunaendelea kuwa na viongozi wanatumia kila njia ili waweviongozi badala ya kuwa na wale wa kuombwa na hata kulazimishwa kuwa viongozi wakijua kwamba uongozi ni kazi nzito inayohitaji kujitoa kuwatumikia wengine?
Kujitambua sisi wenyewe kwanza ili tuweze kuitambua nafasi yetu ni muhimu. Katika maisha yetu tunajua mambo mengi, tunatenda mambo mengi. Tunajua jiografia ya dunia nzima, tunajua sayansi, tunajua aina za vyakula, wanyama na hata nchi na tunatenda katika mkabala huo. Lakini ajabu ni kwamba tunajua kidogo sana au hatujui chochote kuhusu sisi wenyewe – hatujitambui. Maarifa ya kujitafuta na kujigundua ili tujijue sisi wenyewe ndiyo ya msingi kwanza.
Mashuleni na vyuoni tunaandaliwa ili kuwa wazalishaji bora lakini hatufundishwi kuhusu sisi. Ndio maana tunaishia katika tamaa za ufisadi. Tunashindwa kutambua hata chakula stahiki kwa ajili ya miili yetu na hivyo kula hovyo mpaka tunapata magonjwa. Kujua kuhusu sisi au kujitambua ndio msingi. Ni lazima tujijue kwanza ili tuweze kujitedea mema. Bila kujitendea wema sisi wenyewe hatuwezi kuwatendea wema wengine, itakuwa ni ndoto ya mchana
wengi wa watu waliokwisha kuiacha miili (kufa) na kuendelea kukumbukwa walijitahidi kwa kiasi kikubwa kutenda mema, kuwa wema na kuishi kwa faida ya jamii pana. Sio kuwa mafisadi wa kujilimbikizia mali tu. Katika suala la mali tuelewane. Kumiliki mali nyingi sio kubaya, kibaya ni tamaa na kujilimbikizia hovyo hovyo hadi kuishi kwa hofu na kuikosesha jamii mahitaji yake ya msingi.
Amani ya kweli na upendo wa kweli vimo ndani mwetu. Nilazima tuweze kujitambua kwanza na kuishi kiuhalisia ili tuweze kuepuka tamaa, mihemko na vuruu zisizokuwa za lazima. Ni lazima tuyaishi maisha kwa uhalisia badala ya mateso kuishi kwa kugushi na kwa kujikataa. Hata kama unaamini kuna mbingu, kumbuka huwezi kwenda na kufarahia maisha ya huko kama hujaweza kwanza kuyaishi maisha ya hapa ambayotayari uko nayo. Maisha yoyote yajayo yawe ya mbinguni / ahera au hapa duniani, yanategemea yale uliyonayo sasa. Yaishi haya kwanza, jitambue ili ujiheshimu
Sunday, October 4, 2009
msemo wa kizazi cha leo
Friday, October 2, 2009
ukikutana na mpenzi wako wa zamani
sasa sababu iliyionileta Dar ni kusoma japo nilipaswa kwenda Arusha, nikasingizia kutokupata chuo kumbe nilitaka kuwa karibu na aliyekuwa mpenzi wangu NW. hata hivyo alinipiga chini sikuwa naye wala nini
juzi tu nimekutana naye, bint yuleee niliyempenda na kuongea naye kama vile sina haja naye ya kimapenzi tena wala nini. NW aliponiangalia jichoni, nilirejea mwaka 2003 tulipokuwa wapenzi, duh, inakuna mpaka moyoni lakini ndo hivyo, nshajisalimisha kwingine
niliongeanaye kwa muda na kuuliza kulikoni lakini maisha yanaendelea. sikutaka kujua saana kama yuko kwenye uhusiano mwingine kwani hayao ni maisha yake binafsi na siyo yangu. aliniambia anavyofanya kazi katika benki moja ya jijini Dar, nikampongeza na aliniambia anaishi maeneo ya Kinondoni.
sikutaka kupajua anapoishi na wala sikutaka namb a yake ya simu na bahati nzuri mimi sio mteja wa benki anayofanyia kazi. ni maajabu kuwa alilnisabishia kuhamia hapa na sasa ninapojiandaa kuondokanakutana naye tuna.
ni maisha ila ukikutana na mpenzi wako wa siku zote ndugu yangu, ambaya uliwahi kumpenda kiukweli ukweli, hata ujifanye vipi lazima kuna hisia fulanilakini kumbe mambo yalipaswa kuwa kama yalivyo na ndio maana sio wako tena
wakazi wa Musoma, mwanza, kahama na Bukoba, maarifa ya utambuzi yanakuja octoba hii hii, kaa mkao wa kujitambua
Thursday, October 1, 2009
BAADHI TA TUMISEMO TUMEBORESHWA
RAHA YA CHUNGWA, UMENYEWE, KISHA UKATIWE".
RAHA YA NANGA BAHARINI, MTONI ITASHIKWA NA TOPE."
UTAMU WA NDIZI UKO NDANI YA "NGUO" ZAKE.
VUA NIKUPE VITAMU KAMA UTAWEZA KUVUMILIA VIGUMU PIA
Ingawa vingine ingawa hunoga ukivivua lakini waweza pia kuvifunua tu halafu kwa mrija ufyonze juisi ya ndani ya embe iliyobinywabinywa embe sindano.
KULA NANASI KUNAHITAJI NAFASI.......
mwalimu alizoea kusema wavulana juu wasichana chini akiimanisha hosteli za wasichana zilizokuwa sehemu yenye mwinuko na sisi tulikuwa pande nyingine.
mtaka cha uvunguni, sharti ainue kitanda.
aliyekojuu, mfuate huko huko maana hashuki na anazidi kupenda.
asiyesikia la mkuu, masikio yake hayasikii vizuri au hasikilizi.
mwenye macho, anaona vizuri.
akili ninywere, kwa sababu ziko kichwani
Tuesday, September 29, 2009
Mambo ya Bungeni bajameni.

picha hii ni moja kati ya zilizopigwa katika bunge kivuli lililofanyika juma lililopiata pale karimjee. nimejifunza mengi zaidi ni jinsi ya kuendesha shughuli za Bunge na changaoto zake lakini kubwa zaidi nimeona umuhimu wa kuwa na wabunge vijana wenye changamoto lukuki na wenye vichwa motomoto.
kama picha hiyo inavyoonyesha, kuna wakati inabidi mkuu, utoe jicho kwa hasira na huruma lakini uvumilie na kulinda ulimi sijefyatuka kama bloguni. nimejaribu kuweka video lakini inagoma. mngejionea juu ya changamoto za kambi tawala na kambi pinzani na ni kwanini tunahitaji wapinzani wengi bungeni.
kuna mahala spikianalazimika kuliburuza bunge na akizubaa wabunge wa upinzani watamburuza yeye lakini kuna maamuzi mengine ni ya kidiktata kwa sababu za kisiasa au inabidi iwe hivyo. miongozo ya spika ilikuwa kibao. kwakweli ni changamoto na natamani video ikubali.
baada ya hapo tutasema nini kinafuata. nitasafiri kwenda mikoa mitatu ya kanda ya ziwa ikiwemo Shinyanga, Musoma na kagera na baada ya hapo nitatoa msimamo wangu juu ya kile alichokisema mjengwa au matondo.
tunahitaji damu mpya bungeni jamani au sio?
Monday, September 28, 2009
Wezi wanaoiba pesa ya Mungu
basi siku nyingine ikatokea baada ya kukusanya sadaka, wakaja majambazi na bunduki. wakachua sadaka zoote pale madhabahuni na kuwataka wanaibada wasiwafuatilie kwani si walimtoleaMungu? sasa wezi wameamua kuchukua pesa za mungu. Who knows labda Mungu kawaagiza, si miujiza tu ya Mungu ni mikuuu?
pastor akakosa hela ya uji
wiki yanenda kwa usalama barabarani
Thursday, September 24, 2009
niko Bungeni jamani
Wednesday, September 23, 2009
from rwanda with lessons part I
Wiki chache zilizopita niliahidi ku-share na blog hii ya jamii mambo machache niliyoyaona Rwanda. Nilimepata msukumo zaidi kutokana na historia ya Rwanda, kwani mwaka 1994 mauaji ya kimbari yalisababisha mauaji ya watu wengi sana, inakisiwa zaidi ya watu 500,000.From Rwanda with lessons – Part II itafuata.
Mdau IK.
Sunday, September 20, 2009
Ulimi ndo mbaya au?
ulimi kitu kidogo saana
lakini chafanya maajabu.
ulimi wamtukana muumba
natena unamtukuza.
ulimi unavunja unyumba
ulimi watenganisha watu
ulimi wafanana na moto
moto mdogo huunguza pori
ni hatari mwenzangu.
mtu huyo asiyekosa
katika huo usemi wake
basi huyo ndiye mtu mweema
alindaye ulimi wake
ofcoures ulimi ndo unaokula, kunywa maji na kutema makoozi. lakini je ni waajabu labda kuliko viungo vingine kama vile viitwavyo Nyeti a.k.a sehemu za huli (siri)? unaamini kuwa watu wote ni matokeo ya ngono? kipi cha ajabu ulimi au?
Friday, September 18, 2009
Ni wangapi wanaoweza kuridhika?
Ukiwa na waliokuzunguka, hamkosi kutofautiana, ukiwa peke yako, ndani mwako kuna kelele na vurugu kibao. Unatamani kuwasha redio, kusoma kitabu, gazeti au hata msaafu. Au unatoka ili utembeetembee, mambo yanaboa, duh.
Sasa maisha yanaaza kukutishia. Ni magumu, huwezi kukaa peke yako, unatamani uwe na wengine, ukiwa nao, hamkawaii kukosana na kugombana. Na hii ndio sababu familia nyingi zina migogoro. Tunaona makosa kiurahisi kuliko mazuri au hata kusahihishana. Maisha ni ya masharti kweli kweli.
Tunatafuta mali na kujitahidi kumiliki mali nyiiingi zaidi ili tuumiliki ulimwengu na kuna wanaojiaminisha kuwa wanamiliki ulimnwengu kumbe ni mateso matupu. Unafikiri marais na wabunge wana amani yoyote na kuona maana halisi ya maisha? Hawana. Wanatawaliwa na hofu, huzuni ni kuhangaika ili waendelee kuwa madarakani.
Tunakufa kwa presha kwa sababu ya kutaka kumiliki kitu fulani na tunasahanu kwamba kuna kitu muhimu tunachokimiliki ambacho ndicho cha kujivuna nacho kuliko vinginevyovyote viwavyo. Kitu hicho ni sisi wenyewe. Hakuna awezaye kutumiliki sisi isipokuwa sisi wenyewe tunajimiliki. Badala yake tunakimbizana na vile vya nje yetu tukidhani vitatupa furaha kumbe furaha ya kweli imo ndani mwetu.
Ninapopanga kuanza maisha mapya kwa kurudi kijijini, nafikiri itanisaidia sana kuliko kuendelea kutafuta nisichokihitaji hapa mjini. Utafutaji huo kamwe hauwezi kufanikiwa kwani nikipata hiki, natamani kikubwa zaidi kama wewe vile. Kumbe vitu vichache tu vinanitosha na hivyo naweza kuishi bila stress kule vijijini kuliko kuhangaika na kufukuzana mijini.
Au unasemaje wewe. Unadhani ipo siku utaridhika? Hapana na kwa hiyo ni lazima utafanya kazi mpaka uvunjike, utaamua kuiba na kuwa fisadi kwa kuamini utapata furaha na utaishia kufa kwa hofu na ugiligili kwani kamwe hatokipata kile unachokitafuta nje yako, labda urudi ndani mwako ndimo kilimo humo.
AMINA
Thursday, September 17, 2009
Maisha yetu ni kutanga tanga, mpaka lini?
Basi binti alikuwa mitaa ya posta akielekea kazini. Nikaona pia mkanganyiko wa kimaisha ya kila siku. Anaelekea nitokako kama kazini kwake wakati mimi pia naelekeo atokako kuwa ni kazini. Ni maisha. Siwezi kuwa yeye ili niwe karibu na kazi wala kinyume chake.
Kanielezea anavyofanya kazi fulani ya kuingiza takwimu kwenye kompyuta. Ni kazi ya muda mfupi japo inampatia kiasi kikuubwa sana cha pesa. Binti huyo ambaye ni muhitimu katika chuo kikuu cha Dar es salaam kanistua juu ya wasi wasi na hofu ya wanadamu waliowengi ya kukimbiza kilichokuwa mbali nao wakidhania kitawapa furaha kumbe ni noma.
Kanielezea anavyofanya kazi ile lakini anaweza kuachana nayo muda wowote akipata kazi nyingine kwani haina ¨future¨, eti ni ¨temporary¨ n ikaangalia na kushangaa juu ya kawaida yetu ya kuishi kesho badala ya leo na sasa. Anatafuta kazi ya kesho wakati kesho yenyewe hajaiona badala afanye kwanza hii ya sasa. Hajui kama kesho yake inategemea sasa. Ana hofu, ana wasiwasi na majuto
hajui kama kazi ile itamuhakikishia ¨future¨. Ni msomi ni mhitimu wa university of Dar es salaam ana shahada ya BCOM, nzuri tu. Mtu kama huyo hawezi kufanya kazi kwa ufanisi wala kwa moyo kwa kuwa anaitafuta nyingine, si ameishaifikia kesho? Anadhani akipata yenye future itamsaidia sana. Hajui kuwa kuishi kesho wakati bado uko leo ni kujichanganya akili bure.
Msomi huyo wakike na wanawake wanasemekana kuwa noma, eti ukimsomesha mmama basi umesomesha kijiji kizima kuliko libaba levi, zinzi liishilo na mmama huyo huyo. Hajatulia. Anatafuta maisha ya kesho sio ya leo. Hii ndio noma yenyewe. Hana mpango wowote, yeye ni mwanasayansi wa aina yake, anayetaka kuigundua kesho wakati hajamaliza kuiishi sasa (leo)
ndio maana ukimtongoza mdada, mdanganye utamuoa, si anataka maisha ya kesho? Wakati wewe unaitaka sasa! Ndio maana maofisi yetu hayatulii, hayana watu wanaoweza kufanya kazi kwa ufanisi. Kwa sababu wanaitafuta kesho. Wanataka kujua bosi anasemaje juu ya kesho, hafukuzi mtu kweli? Mshahala upo je?
Muhasibu anataka awe meneja wa fedha. Mfanya kazi wa kawaida wa wizarani anataka kuwa naibu katibu mkuu, katibu mkuu anatamani kuwa naibu waziri, na waziri anatamani kuwa Waziri mkuu / raisi. Mwishowe ni kutambika ili wawe mawaziri badala ya kufanya kazi kwa bidii na moyo, wanatamani kesho yao.
Ufanisi wa kazi hamna kabisa. Ni ubabaishaji na hofu juu ya kesho au majuto juu ya jana. Ndoa nazo ndo hivyo. Una hofu kama mwezio hashuguliki na wa nje, utadhani wataondoka naye / nayo. Ni maisha ya hofu saana. Una hofu na kulazimika kuwa mnafiki wa kuishi ili ukifa uende mbinguni na sio kwenda mbinguni kabla ya kufa, si unahofu?
Hao ndio wasomi wetu. Eti wanaitafuta ¨future¨ wakati wanahitajika sasa na sio kesho. Malengo yetu ni kupata vyeo na kula hela na kujilimbikizia mali badala ya kutumika na kufanya kazi kwa malengo kwa faida ya jamii pana. Nikisema ntarudi kijijini kuwa mkulima naonekana chizi. Si mjini ndo kuna mihela?
Wednesday, September 16, 2009
unaaminishwa maisha ni magumu?

mazingira yetu ya jamii tuishimo zinatuaminisha siku zote kuwa maisha ni magumu na sisi tunakubali kwa kiasi kikuuubwa sana.
shule tunaambiwa ni ngumu na siku za mitihani ni vitiisho kwa kwenda mbele. tunashuku uwezo wetu, maongezi na matendo yetu. tunatishiwa juu ya kifo kama vile ukimwi, ajali nk. maisha ni magumu ati.
tunaambiwa hajtujaendelea na uchumi wetu ni mbaya sana nasi tunaamini na kuhangaika. tunaambiwa kuishi karibu na wenye hele ndio kuendelea na ndiyo maana waTZ hujibana DSM na waafrika huzamia na kwenda ulaya na marekani.
tunaambiwa tusipokuwa makini mambo ni mabaya na yanatisha. sasa kuna mporomoko uchumi nao unatutisha utadhani tulishiriki kuujenga. maisha yamekuwa ni ya pesa tu utadhani tulizaliwa na pesa mkononi au bila pesa hakuna maisha.
imetufanya tukaanza kuishi kesho. tunawasiwasi saana na maisha yajayo zaidi kuliko tuliyonayo sasa.
mbaya zaidi tunaenda kwenye nyumba za ibada na kutishiwa juu ya dhambi zetu, Mungu na siku za mwisho eti hizi ndo za mwisho na zikiisha, basi uwezekano wetu wa kuchomwa moto ni mkuu zaidi. inapendeza pale mmoja kati ya waupigao mkwara huu anapokutana na masahibu makuu kuliko yale wakambiayo wewe uyatendeye kuwa ni dhambi. basi wanamaliza soo kiaina kwa kukudanganya kuwa alipitiwa na shetani kumjaribu kama YETHU alivyjaribiwa porini. unaendelea kuwa na hope mkuu.
Anyway, tusipigane mikwara wala huwa na hofu juu ya hili wala lile. kumbuka hatukuomba kuzaliwa bali sis ni matokea ya michezo fulani ya watu wengine na hivyo hivyo maisha ndivyo yalivyo. simpo, ni mchezo mchezo tu wa kupokea kila jambo kam linavyokuja badala ya wasi wasi na hofu za nitakufa lini au ntakula nini. wewe ishi tu kama nikifo kinakuja kivyake huko na kama hakija achana nacho. jamaa yako anakuonaje sio ishu kwani si ulizaliwa peke yako?
usiende misibani kuzika ili nawewe ukifa wakuzike. kumbuka ukishatoka kwenye mwili (kufa) mwili unakuwa ni taka taka ambayo lazima izikiliwe mbali vingevyo ni harafu kali tu. usijali utaziukwa wapi kwani mwili unakuwa sio wako tena na unastahiri kutupwa popote.
dont fear, take it easy dear
Monday, September 14, 2009
ni miaka mitano jijini Dar sasa. bado wakujaehe?
Mwezi kama huu katikati mwaka 2004 ndipo nilipoamia rasimi jiji Dar es salaam.
Mara yangu ya kwanza kabisa kufika jijini humu ilikuwa ni mwaka juni, 2001 nikiwa bado mkristo au mfuasi wa Maltin Luther mzuuri nilitoka kwetu bukoba na kusafiri hadi jijini morrogoro kwa ajili ya mkutano wa kitaifa wa waluteri maarufu kama ”national conference” ambapo tuliimba, kupigwa mikwara juu ya maisha yetu ya baadaye na kufundishwa juu ya ngono (urafiki uchumba na ndoa)
Nikiwa jijini morogoro ambako nilifika kwa treni (ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kuiona treni live na kuisafiria nikiwa daraja la tatu – kukaa) niliamua kufanya mchongo na binamu yangu mmoja aliyeko dar ili nifike jijni humo kwani morooro kulilkuwa na mbu wa kutosha. Basi bwana, kimya kimya bila kijulisha familia, nikajitupa jijini. Nakumbuka ilikuwa siku ya jpili.
Kabla ya kufika jijini humu nilidhani jiji hili lilikuwa la-nguvu
Nilishangaa kuona jiji likiwa limezagaa kila aina ya uchaafu, halitamaniki, mitalo imeziba, limejaa maji machafu na linanuka kila aina ya uozo. Nikadhania labda bado niko Dar vijijiji, akafika jamaa yangu kunipokea, tukaelekea kule home, duh, nikashangaa kumbe Dar watu wanakanyaga udongo! Ile mikogo ya wale jamaa nilidhani huku kuna lami mpaka ndani.
Labda sijafika mujini, tukaenda posta, dah! Sisiemi sana japo niliona maghorofa marefu zaidi. Mkoa wa kagera nilikotokea haunaga matatizo ya umeme kwani umeme unatokaga Uganda. Basi majamaa waliotoka dar wakaja kagera, kila umeme ulipojaribu kukatika, basi ilikuwa gumzo la wiki nzima jinsi mikonai kulivyo hovyo na dar hamna tabu zile, kufika dar nikashangaa mgawo kwa kwenda mbele na hamna umeme mchana mzima. Swali likawa je, yale madoido yako wapi?
Basi bwana, likizo yangu ikamalizika vyema na nikarudi mkoani kwa mbinde. Mwaka 2003 baada ya masomo yangu kule chuoni, nikaja tena Dar, mambo yakawa mazuri kwani nilikutana na msichana N. W, niliyempenda toka Bk akiwa mwanafuzi wa Makongo, basi tukaanza uhusiano raasmi na uongo kibaaao wa nakuota wewe, mara siri, sirari na ahadi za ndoa.
Nikaondoka na kwenda kuanza kazi Bukoba. Wacha nikaasema lazima nikasomee Dar, karibu na N.W mke mtarajiwa, na hivyo kulazimika kuishi nisikukopenda (Dar) kwa sababu kuna ninayedanganya naye kuwa tunapendana (N.W) na kuachana na mpango wangu wa kusomea chuo cha Arusha.
Ulikuwa ni mwanzo wa matatizo kwani nilipokuja mwaka 2004, nilikuta N.W haikubuki tena hata sura yangu wala bangi zangu za kumuoa, kumuota nk, shukuru Mugu sikunywa sumu, vinginevyo usingenisoma hapa leo hii. Dah, yakaisha, nikaanza masomo, nkatamani kwenda Arusha ila kumbuka niliiisha kutelekeza kule kwa ajili ya NW, nikavumilia shida za misongamono ya magari, majumba na hata wingi wa watu chumba kimoja nyumbani, ni maisha tu ya da na joto lake.
Anyway, nilifurahia sana kwani niliishia kujitambua na kuwa ’enlightened’ kupitia initiation ya Santmat meditation. Mpaka sasa nasepa, life is better, tunaendelea kuishi na kusavaivu, badala ya NW nikawapata lukuki, wa mujini, siwawezi nikawa ’singo’ na sasa naendelea vyema
Imepita miaka mitano sasa. Maisha ya hapa ni ya kukimbizana na usiyemuona ya hofu, wasi wasi na misongamano ya kila kitu. Kuna baa nyingi za kujidunga lakini pia kuna maarifa kibao ukiamua kuyatafuta. Makanisa na ulokole ni kabao, na vijiwe pia. Utapeli na uhuni ni wa kutosha lakini michongo pia ni kibao. Nimefahamu mengi hapa ila kuna maisha mengi ya feki na ya kufoji.
Miaka mitano ipitapo ni wakat kuamu kwani nilikuja hapa nikiwa na malengo ya kuishi miaka mitano tu, na sasa ndo hiyooooooooooo imechanganya miguu na kukata kiuno ikitokomea kusikojulikana. Je sasa ni wakati wa kuamia wapi? Mikoa ya kusini, kasikazini au kanda ya ziwa? Kati je? Mashariki je? Au usukumani?
Ua na mimi niende states kwa matondo na kijana wa changamoto nini? No. Au niende Rwanda kwa CHIB? Hapana, kumbuka mpango ni kwenda kwa Yasinta Sweden na kukaa miezi mitatu tu ili nile na kulala bure harafu nirudi huku.
Kwa maoni yako wewe unayeishi mujini na ugenini, unaona ni busara kwanu kurudi kijijini kwetu na kulima na kusaidiana na jamii ya pale au nikae town au niende uzaramoni? Kwa wanyanchoka je? Nafagiia musoma lakini duh, kuna chacha wambura na anajiwwe mfukoni muda wote! Aha ukiangalia negativuz utakuwa sio mwanaume.
Sijui kama niende maulaya na kuanza kikimbizana na Muda ili muda uwe bosi wangu huku nikihaha kupata kilichombali au nisichoweza kukipata na hata nikikipata hakinipi ridhiko na naendelea kukimbiza kingine? Muhimu: ni wakatai wa kuondoka Dar, sijui niende wapi bado, nichgulieni
Friday, September 11, 2009
Wednesday, September 9, 2009
kuongeza Nywere na makalio, wazdhungu kuota jua

katika post moja wapo hapa kijiweni, tulizungumzia juu ya wadhungu kupenda uafrika na waafrika kupenda udhungu. chib aliongelea juu ya wadhungu kujianika juani wawe kama weusi, na weusi kujiharibu ili wawe kama wadhungu na kutumia manyoya ya paka ili nywere zao ´zidhunguke´
Chacha wambura akaongelea mikongóto ya wanawake watakaomsikiliza yule dada mwenye Suruali mbanano na Yasinta akasikitishwa na utamaduni wetu kufa. anyway tukasikia magazetini kuwa mke wa kigogo mmmoja yuko hatarini kwa matako yake a.k.a makalio kupinda pinda hovyo.
yote kwa yote. sijui niite nini. ni ile ile kijana wa changamoto aitayo kujipoteza katika kujitafuta. wadhungu wanapojaribu kufanana na waafrika hawajipotezi, bali wanajipata vizuri tu. wanasuka nywere na kumbuka kusuka hakuna soo yoyote ile zaidi ya kuuwaepusha na makemikali vichwani mwao.
kujianika juani ni faida kwa kila afanyaye hivyo japo wengine huwa tunalikimbia na kuliona linatutia nuksi. niliwahi kuandika makala juu ya uhusiano wa karibu kati ya jua naMungu a.k.a muumbaji a.k.a nguvu kuu. wadhungu kule kwao hawalioni jua. na labda baridi ndio inayowafanya kuwa weupe vile. kuupata weusi ni dili kwani ni rahisi tu, ni kwa kujianika juani. lakini weupe sio dili kwani lazima hujiaribu na kujiingiza matatizoni ili uupate weupe.
na labda ngozi nyeusi ndio dili kwani inajidhihirisha jinsirangi hii isivyobadilika kufuatana na hali ya hewa bali iko vile vile, kwa kiingereza ni constant. lakini nyeupe inabadilika usiku, asubuhi, mchana nk.
kuhusu wadhungu kujianika juani, kumbuka jua ni kani (force) kuu ya asili (great force of nature) kwa wanaojitafuta na kujigundua katika tahajudi (meditation) wanaweza kutwambia nguvu waipatayo kwa kuliangalia jua au kutahajudi wakiwa juani. mchunguze mdhungu au mtu yeyote mwenye tabia za kujianika juani, utaugumdua faida lukuki. hana msongo wa mawazo wala visasi vya hapa na pale. anafuruha na anafanya kazi kwa bidii kwani akili yake huwa freshi. hatulitumii jua ipasavyo kwani hatujui umuhimu wake!
kwa hiyo basi, wajinga na wasiojijua ndo hutumia vitu vya ajabu ili waonekane namna gani vipi. wanapenda udhungu, ni noma wanavaa mawigi na manyoya ya waliokufa. wanakula sumu ili wanenepesha matako yao. sijui kama wanamkosoa muumba ua vipi.
mbaya zaidi ni kwamba hawajifunzi kutoka kwa waliowatangulia. jijini dar kuwa mfano, kuna wamama kibao wameungua nyuso na ngozi. ukiwaangalia ni kama wamechanganyikiwa au akili zao hazifanyi kazi vizuri. wengine wamezaa watoto vilema, zombie nk kwa sababu ya kemikali hizo.
wanajipoteza katika kujitafuta, wanatafuta uzuri, wanashindwa kujua kuwa uzuri wao umo ndani mwao na sio kemikali. uzuri wa Afrika ni kuishi juani miezi kuminambili na kuwa na rangi nzuuuri ya weusi na sio kujipodoa na kujichubua na ujinga mwingine.
ni hayo tu
Monday, September 7, 2009
utamaduni wetu na dada zetu
Jangwa la sahara kuwa kijani,
Sunday, September 6, 2009
"Coloured people are not allowed here.
"The black man turned around and stood up. He then said:
"When I was born I was black,"
"When I grew up I was black,"
"When I'm sick I'm black,"
"When I go in the sun I'm black,"
"When I'm cold I'm black,"
"When I die I'll be black."
"But you sir..."
"When you're born you're pink,"
"When you're sick, you're green,"
"When you go in the sun you turn red,"
"When you're cold you turn blue,""And when you die you turn purple."
"And you have the nerve to call me coloured"
The black man then sat back down and the white man walked away.
Thursday, September 3, 2009
nimeulizwa swali juu ya uwepo wetu
bro, habari za leo, hivi kwa nini tupo hapa duniani? au tupo bila sababu? yaani sisi kama sisitunanufaika vipi na uwepo wetu hapa duniani na kama tupo sio kwa faida yetu, tupokwa faida ya nani?na kama ni kwa faida yetu ni ipi? na kama sio kwa faida yetu ni kwa faida ya akini nani? na nikwanini kwa ajili ya hao wengine kama tupo ajili yao? nimesindwa kujua kwa sababu baada ya mwanadamu kuucha mwili (kufa) sijui ananufaika nini na uwepo wake hapa duniani.
na sms nyingine ni....
uwepo wetu hapa duniani maanake ni nini?, faida ni kwa ajili y a nani? ni kwa ajili mwili? na je faaida hiyo ni ipi?
sms ya mwisho ilikuwa.......
hatujui sababu hasa ya uwepo wetu? sisi kuwepo tupo kwa sababu tumetakiwa kuwepo tu na maumbile?
wewe msomaji sijui kama unajiuliza maswali kama haya au una majibu walau kidoogo kwa ajili ya mwenzetu huyu. karibuni kuchangia.
Wednesday, September 2, 2009
nimepokea ka kwizi haka......
1. How do you put a giraffe into a refrigerator?Stop and think about it and decide on your answer before you scroll down. The correct answer is: Open the refrigerator, put in the giraffe, and close the door. This question tests whether you tend to do simple things in an overly complicated way.
2 How do you put an elephant into a refrigerator?Did you say, Open the refrigerator, put in the elephant, and close the refrigerator? Wrong Answer. Correct Answer: Open the refrigerator, take out the giraffe, put in the elephant and close the door. This tests your ability to think through the repercussions of your previous actions.
3. The Lion King is hosting an animal conference. All the animalsattend .... Except one.Which animal does not attend?Correct Answer : The Elephant. The elephant is in the refrigerator. You just put him in there. This tests your memory. Okay, even if you did not answer the first three questions correctly, you still have one more chance to show your true abilities.
4. There is a river you must cross but it is used by crocodiles, andyou do not have a boat. How do you manage it?Correct Answer:? You jump into the river and swim across. Have you not been listening? All the crocodiles are attending the Animal Meeting.
This tests whether you learn quickly from your mistakes.According to AndersonConsulting Worldwide, around 90% of theProfessionalsthey tested got all questions wrong, but many preschoolers got several correct answers. AndersonConsulting says this conclusively disproves the theory that most professionals do not have the brains of a four-year-old.Send this out to frustrate all of your smart friends.
PS: Just the fact that I sent it to you should make you feel good.__________________________________________________________________________________________________________________________________________
Don’t ask the Lord to guide your footsteps if you’re not willing to move your feet.
Monday, August 31, 2009
jamani nimerushiwa li-dongo
Nyie mnaojaribu kufanya discussion na Kamala mnapoteza muda wenu bure. Huwezi kufanya discussion na mtu asiyejali ideas na ideals za wengine. He doesn't care about your views, life experiences, life philosophy etc. As long as hujui hii DOGMA yake ya kujitambua basi utaishia kutukanwa, kubezwa na kudharauliwa. Angalia comments zake anywhere on the blog world. It is all about this stupidity thing called kujitambua (the same thing that is preached by the SCIENTOLOGY cult), "teaching" people how to be rich while himself is poor (although he will claim that in kujitambua sense he is rich). Hata utoe points na hoja namna gani as long as siyo mtu wa kujitambua you will be treated as a stupid person. So people don't waste your time trying to argue with a person who thinks he knows everything (in essence a STUPID person) because you may also end up looking even more stupid! Tchao!
Sunday, August 30, 2009
Friday, August 28, 2009
Picha hiyo
bila ridhaa ya Makande masangu nimeamua kuweka picha hii iliyopendeza ya masereburity hao ikiwa na nyuso za furha zilizotpanbwa zikapambika hasa hako kadogo kuliko wote pichani, I like anges si mnajua watoto ni malaika na biblia inasema muwe kama wao ili muweze kwenda alikoenda yesu??
hii ni baada ya kazi za kusafiri na safari ndeefu ya kurejea jijini. tuonane juma lijalo katika mada mfululizo na muedelezo.
asante kwa kuchagua kijiweni blogi
Thursday, August 27, 2009
mara yangu ya kwanza kukutana na kijana wa Changamoto
baadaye nilishangaa kumuona anablogu na kumuuliza kama ni yeyekweli nimfahamuye naye akakiri ndiye. mpaka sasa najiuliza ilikuwaje nikakutana naye kwenye ile nyumba tulimokutana. anywei, nimepost baada ya kuwa hapa hotelini na kuvisiti ka-kompyuta na kuona umuhimu wa kuuliza swali la kwanini pale lakini pia kumuonyesha kijana wa Changamoto mzima mzima.
Wednesday, August 26, 2009
wahubiri wetu na siku za mwisho
hayo ni maneno yanayosikika kwenye Nyumba za ibada. mchungaji mmoja aliwahi kunipiga huo mkwara, aliponitambulisha kwa mke wake, yule mama ailikuwa na mimba. sasa kama ni siku za mwisho kwa nini anampachika mke wake mimba? siaache twafa? au
kwanini anawasemea wale anaodhani wanatenda dhambi?
eti watalia na kusaga meno, wasio na meno je watasaga nini?
wewe kama bado unawaamini hawa majamaaa, du!!!
Tuesday, August 25, 2009
Musoma kwa ajili ya utambuzi.
mnyanchoka
tumefika mikoa ya kanda ya ziwa kwa ajili ya utambuzi. sasa niko mjini musoma Katika ofisi za Foundation help itakapofanyikia semina ya utambuzi mchana huu.
niliwasili mjini msoma usiku wa kuamkia leo mida ya saa sita na nusu nikitokea jijini Dar kwa basi la Mohammed trans. kwakweli nashukuru sana oungozi wa basi hili kwani huduma zao ni nzuuri sana na magari yao yametulia. safari ilipendeza na tulifika salama.
ndani ya basi,karibu na nilipokaa, alikaa mmama ana watoto watatu. ilipokuwa jioni watoto wakataka kulala na mmoja ikabidi aje kwangu kwani nilipokaa kulikuwako na kiti kisichokuwa na mtu. basi katoto kalisinzia kwa shida kwani basi linaruka bumps, ilibidi nikapakate kalale vyema, nilifurahi kuwa mlezi.
mji wa musoma ni mwema, unapendeza. uko karibu na ziwa victoria una miinuko kibao na hali ya hewa n nzuri. ni furaha kumeditate ukiwa mjini hapa
chakula ni kizuri pia na haswa vegeterian diet. sukuru Mungu sijakutana na Wanyanchori wala Wanyanchoka isipokuwa Chacha Wambura marwa!! ambaye hatambei na panga, rungu wala Mkuki.
nawakaribisheni katika semina hii. Kesho itakuwa ni jijini Mwanza
Sunday, August 23, 2009
ni semina za Utambuzi kanda ya ziwa
jumaane ya tarehe 25/08/2009 kuanzia saa kumi jioni semina ya jitambue itafanyika kati kati ya mji wa Musoma, mahala atakapopanga Chacha Wambura.
kwa wanaopanga kuhudhuria Semina hiyo wawasiliane na Bwana Wambura kwa simu namba; 0713 235146 au 0787 945414 ili kujiandikisha na kujua mahala itakapofanyika semina hiyo.
na Jijini Mwanza tutakuwepo siku ya Jumatano tarehe 26/8/2009. Siku itakayofuata yaani Alhamis, tutakutana katika hotel ya Impala na kujaadili juu ya Mungu na Santmat meditation wakati siku ya ijumaa tutaendelea semina ya utambuzi.
kwa walioko mwanza pia wasiliana na Chacha Wambura kwa namba hizo pale juu au piga 0754 771 601 wale wasioweza kuhudhuria kwa muda uliopangwa waweza kukutana kwa muda maalumu kwa kupanga na watoa mada.
Geita na Shinyanga, tuwasiliane kwani maandalizi ya huko bado yapo jikoni
karibuni tujifuze, karibuni tukue
........ kwaniaba ya familia ya jitambue (FAJI)
Dar es salaam
Thursday, August 20, 2009
sipiritual planes
Wednesday, August 19, 2009
Tunahitaji viongozi waliojitambua.
Wakati huo tunapoelekea na kujiandaa kuchagua viongozi wapya wa karibia ngazi zote, ni vyema tukaangalia, tukatafiti na kujiuliza tunahitaji kuongozwa na mtu wa namna gani na aina gani. Tunahitaji kuongozwa na watu waliojitambua kwa ungozi endeleva na wenye tija na sio kuongozwa tu kwa sababu kuna nafasi za kuongozwa na wala sio kuwa na wagombea eti kwa sababu kuna nafasi za kugombea kama ilivyo kuwaida yetu sasa.
Ni wakati wa mabadiliko, ni wakati wa kujitafiti kwanza kabla ya kusimama na kutaka kuongoza wengine. Je, ni kweli sisi tunaoogombea nafasi za uongozi, tuna sifa hizo kweli za kuwaongoza wengine? Kwa nini tunataka kuongoza? Je sisi tunaowania nafasi hizo, tunaweza kujiongoza sisi wenyewe kwa ufasaha makini?
Kujitambua na kuongozwa na viongozi waliojitambua ni jambo muhimu sana . Tunahitaji kiongozi anayetambua kuwa yeye kama binadamu, hapa duniani anapita tu na muda wa kukaa hapa ni mfupi na hivyo tunahitwa kutenda mema sio kujilimbikizia mali . Tunahaitaji kiongozi anayejitambua na kujua mazingira yake. Kiongozi ni lazima ajidhibiti kimwili, kiakili, kihisia na hivyo kukua kiroho.
Tunahitaji kiongozi atakayeweza kuona umoja wetu kama binadamu na sio kubaguana kwa misingi ya ukabila, rangi wala taifa. Tunahitaji kuwa na kiongozi aliyekua (evolve) ni hivyo kuwa juu ya dini ili azimiliki na kuzitawala zote badala ya kiongozi anayetawaliwa kwa kudhibitiwa na dini moja tu ili aone ukweli mpana kuwa lengo la dini zote ni moja.
Tunahaitaji kiongozi mwenye upendo anayetambua umuhimu wa kuwapenda watanzania wote na kusimamia ugawanaji wa rasilimali zote kwa ajili ya wote badala ya kujilimbikiza yeye na familia yake. Ni kiongozi atakayeona utu, umoja na amani kuwa muhimu kuliko vinginevyo vyote. Ni kiongozi atakayeweza kusisitiza na kupanga mikakati yenye lengo la kunufaisha wananchi waliowengi badala ya kujitengenezea tenipasenti yake.
Kiongozi bora ni yule anayekula chakula bora kwa ajili ya afya bora badala ya yule anayekula kwa hisia za kusaka radha ya mdomoni idumuyo kwa sekunde mbili huku akijaza tumbo na kulipa kazi ngumu ya kubeba mzigo usiohitajika na kulemewa huku akikabiliwa na afya mbovu itaanayo na kula hovyo.
Tunahitaji kiongozi atakayeona utumwa uliomo katika kuongoza watu badala ya ukuu usiokuwa ukuu wa maana. Kiongozi mwenye kuingia katika uongozi akiwa amebeba malengo ya kwelli ambayo kwa nia na moyo waka anaamua kuyatetea, kuyaamini na kuyafanyia kazi na sio kiongozi wa kuandaa propaganda za kudanganya wapiga kura ili wampatia ulaji. Kiongozi anayeishi miongoni mwa jamii anayoiongozi na sio mkazi wa ‘mujini’
Je! Kiongozi huyo atatoka wapi?
Bila shaka ni miongoni mwa jamii yetu. Jamii ya wapigakura wetu inapaswa kujitambua, kuwa na malengo na kumtambua yule atakayeweza kweli kuwafikisha katika malengo yao . Jamii hiyo ya wapigakura haitasubili hata siku moja waje wale wajanja wa kujua kuchonga maneno na kujifanya wanajua shida na mahitaji ya wananchi hivyo wawachague ili waishi kwa ahadi na ndoto za mchana, bali jamii hii itawatafuta wale inaoamini kuwa ni bora na kuwaomba kwa njia yoyote hata kama hawataki kuwa wawe viongozi wao.
Jamii itatambua kuwa viongozi wa kweli huwa hawapendi kuongoza na hivyo itajua umuhimu wa kuwaomba na kuwasihi wafanye kazi hiyo. Jamii iliyojitambua kiasi cha kuweza kuwa pamoja na kujua nani wa kuwaongoza, haitakuja tu, bali itatokana na vyombo vya habari makini. Si vyombo vya habari vya kuandika habari za kushutusha kutishiana bali vinavyoandika habari kwa lengo la kaelimisha, kuhamasisha na kuwaonesha wananchi umuhimu na nafasi yao katika kutatua yanayoitatiza.
Mwisho wa siku tutapata uongozi wa maana, wa kueleweka, uliowa kwetu na wakutufaa. Vinginevyo tutaendelea kuwapigia kura watalii katika majimbo yetu na nchi yetu, watakaokuwa wanasimamia na kutunga sera za elimu huku wakisomesha watoto wao ughaibuni, tutaendelea kuwachagua wachoyo wasiojua wanacho kihitaji na hivyo kujikusanyia kila wakionacho machoni pao. Tutaendelea kuwachagua wanafiki wanaoona makosa ya wenzao huku wao wakipata nafaasi hushindwa kuyaona yale waliyoyaona walipokuwa nje ya uongozi
Monday, August 17, 2009
semina ya utambuzi jijini Mwanza!
kutakuwepo na semina ya utambuzi jijini mwanza kwa muda wa karibia juma zima kuanzia siku ya jumanee tarehe 24/8/2009. semina itakuwa iikifanyika mida tofauti kufuatana na upatikanaji wa nafasi wa washiriki na mahali pa kufanyika semina hiiyo patajulishwa baadaye.
yatakayojadiliwa ni pamoja na:
Namna ya kupata utajiri pamoja na mafanikio katika biashara, kiuchumi, kazini na shuleni; namna ya kujenga mahusiano mema kazini na upendo wa kweli katika ndoa, suluhu ya tendo la ndoa; namna ya kujiamini; kuondoa msongo wa mawazo, chuki, kijicho na hasira za ziada; kinga ya uchawi; namna ya kupata chochote utakacho maishani; kuondoa tabia sugu kama ulevi, uvutaji sigara n.k., kuondoa hofu na aibu, kupata afya nzuri kimwili kwa njia ya tiba mbadala, kufikiri vizuri, n.k.
wale wote watakaoweza kushiriki semina hii wawasiliane kwa kupiga simu namba, 0754 771 601, email; utambuzi1@yahoo.com au utambuzi1@gmail.com
hakuna kiingilio maalumu japo inaruhusiwa kutuoa mchango kwa watakaojisikia.
ahasanteni sana na karibuni wakazi wote wa Mwanza na vitongoji vyake.
Ahsanteni.
imetolewa na afisa program,
FAMILIA YA JITAMBUE (FAJI)
Sunday, August 16, 2009
Ajira zetu na mikopo ya kudhalilishana.
Kwamba hata tulichonacho tunaking’ang’ania hatuko tayari kukiachia huki tukikimbiza kilichoko mbali tukiamini kitatupa furaha na ridhiko. Hayo ndiyo maisha yetu binadamu wa leo katika ulimwengu huu. Hatuishi sasa bali tunaishi jana na kesho. Tumeiacha sasa ijiendee ipendavyo wakati ndiyo halali yetu.
Mtoto akizaliwa anaambiwa asome ili apate maisha mazuri utadhani wasio soma wana maisha mabaya wakati ulimwengu ulibadirishwa na wasiosoma zaidi ya wasomi, na anachaguliwa cha kusomea na wazazi wake badala ya yeye mwenyewe kuchagua apendalo na siku zote huambiwa maishani magumu wakati hata wanaomwambia hivyo bado wa naishi sasa kama ni magumu mbona nyi mnanishi?
Kila siku kabla ya kuendeleza shuguli zangu na haraka baada ya meditations zangu, huwa naomgea na jamaa yangu kwa jina joram. Tunaongea mengi juu ya maisha kwa kuangalia hali halisi. Huwa tunaketi karibu na parking moja ya magari ya jamaa wafanyao kazi ofisini. Basi siku hiyo tukawa tumeyaangalia magari, jinsi yanavyoegeshwa na kubaki vile, kwa kweli yanapendeza.
Unajua nini? Wafanyakazi wana magari mazuri kwa kweli. Lakini je, sote tunahitaji magari? Hapana! Waajiri wa sekta binafsi wanatupumbaza na kutufanya kuwa tegemezi daima kwao. Wengi wa waajiri hao hutoa mikopa (wakati mwingine) ya lazima kwa wafanyakazi wao ya magari. Inafika hatua ukibadili kazi, basi mwajiri mpya anakununua wewe na mkopo wako ukamfanyie kazi.
Eti mtu anakukopesha gari tena la kifahali na unalilipia hela kidogo huku ukijiona umeula! Sehemu ya mshahara inaelekea kulipa gharama za gari lako. Kusema kweli unaanza kulihudumia gari kwa kulinunulia mafuta, kulilinda na kulikarabati na hivyo sehemu ya mshahara hiyo kwenye gari. Kumbe jamaa kakukopesha gari ili uwahi kazini au akikutuma basi ufanye shuta.
Baada ya miaka mitatu au mine gari lako hilooo limechoka na kupitwa na wakati na hivyo linakugharimu kulitengeneza au kuliuza kwa hasara na ni wakati huo umemalizia au hujamalizia kulilipia, si ni mkopo tu ule? Kwa hiyo unalipia kisichokuwepo au unalipia unachokilipa tena!
Mwisho wa siku sio wewe wala gari, umeliwa. Hata wakati mwingine huna ela ya mafuta ya kuendesha gari lenyewe. Sijui utachukua mkopo. Pesa ambayo ungeitumia wasomesha wadogo, watoto, ndugu nk, zimeshia kweenye gari ili wakuone kuwa na wewe una gari! Maisha ya show, ni noma.
Rafiki yangu Joram ambaya ni mfanyakazi mwenye cheo serikalini, yeye hataki mkopo wa gari wala kununua gari kwa pesa zake hata kama anauwezo huo kwani anaamini magari yoote ni yake. Dala dala, Tex hata mgari binafsi yampayo lift yanamtosha sana kuliko kununua la kwake binafsi.
Labda ndio maisha yetu hayo ya mbio za panya, ‘rat race’ wakati tunaenda kanisani kumshukuru ‘mungu kichaa wetu’ kwa kutupatia magari mazuri, interesting ehe? Tunahitaji nini haswa sisi? Kipi kitangulie? Gari, mke,nyumba, computer, wanyama au?
Friday, August 14, 2009
maisha bora yashafika hamyaoni?

wengi mlikuwa mkisubilia wanasiasa waje na maisha bora kwa kila mbongo kama walivyoahidi. sasa huu ndio wakati wenyewe sasa. nauli za mabasi ya mikoni zimeshuka na zinaendelea kushuka kwa kisingizio kuwa bei ya mafuta nayo imeshuka. inasemekana nauli za dala dala nazo zitapungua kati ya Sh 50 mpaka 100.
si mafuta yameshashuka bei? wakuu wa mikoa wamebadirishwa ili kuondoa sura za kamatakamata ile mamantilie machinga nk. kubwa zaidi mkuu wa mkoa wa Dar, Willy Lukuvi, ameisha tangaza kuwazuia wale Mugambo wote waliokuwa wakiwapiga akina mama na kuwavua nguo machingazi.
amewapiga marufuku kwamba kazi yao sio njema na kuipaka matope kibao kiasi kwamba ukiwashitaki wanaweza kufungwa maisha au kama vile serikali ilikuwa nje ya nchi wakati wanafanya unyama ule! nakwambia mambo ni mazuri sasa kwani bidhaa zitapungua bei zaidi na zaidi.
machinga wanarudi mitaani. nilikuwa Bukoba, wale jamaa wanaosafirisha kwa piki piki (maarufa kama Asekido / boda boda) wamesheheni mitaani na wanafanya kazi bila wasi wasi wala bugdha. mambo mazuri hayo. bila shaka bei za mazao zitapanda na mkulima atakuwa hurukuuza apendako. kama unatak
a kujiunga na elimu ya juu huu ndio weakati kwani nakuhakikishia kuwa watakaodahiriwa mwaka huu watalipiwa gharama zote na wale wa mwaka kesho (full sponsord) kwani wakati wa kampeni zilizopita nilikuwa mwanachuo na sikuwa na sifa za kupata mkopo lakini tulipata sote na ni full! Jiunge mzee. kama unataka kuanzisha biashara huu ndio wakati kwani hata usipofuata kanuni sawatu na twende mbele. ni wakati wa kuvuna matunda ya uongozi na ni wakati wa kuyaona maisha booooora kwa kila Mdanganyika.mzee wa changamoto huwa haelewi inakuwaje wanasiasa, sasa hili ndilo jibu. kabla ya januari mwakani, utakuwa na kila sababu ya kuendelea kuichagua sisiem na viongozi wake. mbuzi wa kafara walee mahakamani. nakuhaikikishia wengi watafungwa japo waweza usiwaone tena.
mramba, Yona, Mgonja, Liyumba, Zombe, Richmonduli, nk. ni wakati wa kuonja joto ya jiwe kwa makosa yao japo mwisho wao ni vigumu kwako kuusikia. mambo ya politikisi hayo nisiyopenda saana kuyaongelea. ila huu ni wakati wa neema na wakati wa dili. ile ahadi ya mabasi yaendayo kasi kwa Dar!!!!!
tutaanza kukabana tena koo kwa kutimuana na kusaini mikataba ya Hovyo mwanzoni mwa 2011. politiks
Thursday, August 13, 2009
rich dad na wajuzi wa mambo
There are so many "intelligent" people who argue or defend when a new idea clashes with the way they think. In this case, their so-called "intelligence" combined with "arrogance" equals "ignorance". Each of us knows people who are highly educated, or believe they are smart, but their balance sheet paints a different picture. A truly intelligent person welcomes new ideas, for new ideas can add to the synergy of other accumulated ideas. Listening is more important than talking. If that was not true, God would not have given us two ears and only one mouth. Too many people think with their mouth instead of listening to absorb new ideas and possibilities. They argue instead of asking questions
Wednesday, August 12, 2009
maisha ya Dar ni kurudi nyuma nyuma tu
kwa miaka yote hiyo, masha ya Dar ni ya ajabu sana. kinachoniacho hoi ni reverse au kwenda kinyume nyume kwani kila kitu kinarudi nyuma na labda yangetengenezwa magari ya kurudi kinyume pekee,. ishu ni Muda wa kuwahi asubuhi.
nikiwa mwanachuo wa IFM, nililazimika angalau saamoja kamili niwe kituoni ili niweze kupata gari ya kuwahi mjini na kuwahi msongamano wa magari. baadaye ikawa saa kumi nambili na nusu, ikaja saa kumi nambili kamili na sasa ni saa kumi na moja na nusu.
kama unafanya kazi zako mjini na usafiri muhimu kwako ni dala dala, basi wewe wahi tu mapema yaani saa kumi na moja asubuhi uwe kituoni vinginevyo utapitia dirishani. ukitaka kupanda dala dala inabidi uwe na nguvu vinginevyo uruke dirishani. hata kama unagari binafsi foleni utakona nazo. ukimaliza zengwe la foleni basi parking ni ishu kwako. mjini hakuna parking na zikiwepo basi hazina usalama.
nyumbani nako vijumba vyetu vimebanana. vimejengwa bila parking kwa hiyo baada ya kufika nyumbani na gari lako, inabidi upige rivasi ya kuelekea kwenye parking ili ulaze gari lako vyema. yaani maisha ya Dar inabidi urudi nyuma nyuma ili mambo yaende. itafika wakati (nao sasa waja) ambao wakazi wa Dar watalazimika kuwa wanaamka saa tisa usiku ili kuwahi town.
yaani inauma. nipandapo dala dala huwa napanda na vitoto vya shule. hivi huwa vinachapa usingizi kama viko home vile kwani uamshwa kabla ya wakati uliopangwa kwao kulala kumalizika. ndoa hazina maana jijini dar na hivyo wanandoa hawajuani kwani muda woote mko safarini ya kwenda msikofika.
nyumbani na chumbani kila kitu inabidi mfanye fasta ili time isichelewe. kwa hiyo mnafanya mambo yenu kama vile mmeibana au mnaogopa kufumaniwa wakati nyie ni wanandoa halali. watoto wanalelewa na mahosegel na hawawajui wazazi wao vyema. si huja wamelala na huondoka wameamka?
ni maisha ya Dar, ni ya kinyume nyume tu yaani reverse. tumechagua kuishia barabarani na tuendako tukifika tunagundua hatujafika bali inabidi tuendelee tu kwenda na kwendaa. labda tutafika!
Tuesday, August 11, 2009
shairi la Mtanga
nimeamua kulitundika ili tulipitie tena.....
Nashika kalamu yangu, salamu nazituma,Kwenu marafiki zangu, natumai mu wazima,Nawaombea kwa Mungu, mjaliwe yalo mema, Salamu wanablog.Simon Kitururu, huzamia MAWAZONI,Fikra zake ni huru, pia zina burudani,Nasi tunamshukuru, hachoki tangu zamani,Salamu wanablog.Yupo dadetu Yasinta, yeye hupenda MAISHA,Kamwe hawezi kusita, mazuri kutuonesha,Sifa tele azipata, maana huelimisha,Salamu wanablog.Christian Bwaya yupo, hutaka tuJIELEWE,Daima aandikapo, vichwa vyetu tusuguwe,Ukweli daima upo, muhimu ujadiliwe,Salamu wanablog.Mubelwa Bandio pia, MZEE WA CHANGAMOTO,Haishi kutuambia, mambo yalo motomoto,Muziki hutupatia, yenye midundo mizito,Salamu wanablog.Subi dada yetu sote, wa NUKTA SABA SABA,Ili mengi tuyapate, blog yake yashiba,Asichoke asisite, ajaze hata kibaba,Salamu wanablog.Chib naye ni rafiki, hutumia HADUBINI,Kazi yake haichoki, popote ulimwenguni,Magharibi mashariki, hutujuza kulikoni,Salamu wanablog.MWANAMALENGA Kissima, hutuonesha MWANGAZA,Makala zenye hekima, na mambo kuyachunguza,Kwa ushairi ni vema, tungo zake zapendeza,Salamu wanablog.Serina Serina huyo, ana UPANDE MWINGINE,Yale ayaandikayo, hupendwa nao wengine,Kwa mawazo si mchoyo, hufanya tushikamane,Salamu wanablog.Koero Mkundi pia, hutuambia VUKANI,Hachoki kutuletea, yatokeayo nchini,Daima hukumbushia, tutoke usingizini,Salamu wanablog.Ndugu yetu Mumyhery, kabobea kwa MAVAZI,Vitu vyake ni vizuri, hilo mbona lipo wazi,Yupo kwenye mstari, hachoki kufanya kazi,Salamu wanablog.Kamala tunamjua, wa nyegerage KIJIWENI,Fikra apambanua, ili tutoke kizani,Sote tukajitambua, tujijue kina nani,Salamu wanablog.Masangu wa Nzunzullima, CHAKULA chake KITAMU,Hatosahau daima, kutupa yote muhimu,Ujuzi wake kisima, haisaliti elimu,Salamu wanablog.Markus Mpangala, KARIBUNI sana NYASA,Yeye wala hajalala, mengi ameshayaasa,Kabobea mijadala, ya jamii na siasa,Salamu wanablog.Lumadede mshairi, USHAIRI MAMBOLEO,Mashairiye mazuri, tena yale ya kileo,Huukuza ushairi, na kuupa mwelekeo,Salamu wanablog.Na MWANASOSHOLOJIA, siachi kumsifia,Elimu kutugawia, na picha kutuwekea,Mazuri hutuambia, ndani ya hii dunia,Salamu wanablog.Nami MWANANCHI MIMI, wa DIWANI YA FADHILI,Tungo zangu siwanyimi, nawapenda kiukweli,Tena mara kumi kumi, tena na kwa kila hali,Salamu wanablog.Ambao sijawataja, lipo shairi jingine,Sote tungali pamoja, kwa mema tuombeane,Tusichoke zetu hoja, hivyo na tushikamane,Salamu wanablog.
Saturday, August 8, 2009
busara za shaaban Robert
Mwaminifu kama mchana, msiri kama usiku
Ulimwengu umewateua watu wachache kama watu bora
Yawezekana mimi ni mjinga, bali fikra yangu ndivyo innavyoniongoza
Ukiwa na fedha utajuta, ukiwa huna utajuta pia, cha nini kitu hiki?
Mauti yaliweza kuwatoa wapenzi machoni pake, kamwe hayakuweza kuwatoa moyoni mwake
Siifu jambo ilipendalo kwa sifa upendayo lakini matokeo yake huwa mamoja siku zote.
Kwa kuwa nimebaki peke yangu sasa, naweza kutenda nipendavyo bila lazima ya kufikiri habari za mtu mwingine
Kila mtu anahangahika shughulika kupata kilichokuwa mbali (tajiri, masikini, wagonjwa, wazima nk) mbali kabisa kama zilivyokuwa nyota za mbinguni
Moyo wa mtu ni msitu mkubwa
Mfalme huchukua raia kuwa malkia wake na malkia huchagua raia akawa mume wake, matajiri huoa masikini na masikini huolewa na matajiri.
Kukatariwa hutia hasira, uchungu, uzni na hata msiba moyoni lakini kufikiria hatua ya kujiua ni upuuzi.
Hapana mwanaume mbaya kwa wanawake wote wala hakuna mwanamke mzuri kwa wanaume wote, mkimkosa huyu utampata yule.
Ufunguo mdogo hufungua kufuli kubwa na mlango mkubwa komeo lake dogo. Kadhalika ubongo wakia chanche katika kicho cha mwanadamu ni kurasa zilizohifadhi fikra zisizo na mwisho
Adam alishindwa kufanya kazi yake borra na akafukuzwa Eden
Sioni akili kusema kuwa neno Fulani haliwezekani eti kwa sababu watangullizi wake walishindwa kulitenda.
Hakuna roho kongwe
Moyo wake ni kama mtoto asiyejua bugdha
Asili yetu ina nguvu kubwa katika mioyo yetu.
Asipojaribu kutendo neno/wazo, utakufa bila kutenda kitu chochote katika dunia.
Miguu ya mtu, humwongoza katika neno lililo katika moyo wake
Humwaziaye harusi, hukuwazia matanga.
Mapenzi ya mwisho ndiyo yaliyo bora
Ndoa ni jambo kubwa sana kwa wanawake, ndio maana hawataki kuingia kabla ya kufkiri sana.
Pang’okapo jina pana pengo, lakini haidhuru.
Pengo la jino moja, halizuii kinywa kutafuna.
Siri ni kitu kimoja katika vitu vinavyotisha.
Kutafuta furaha maishani ni kama kumtafuta paka mweusi katika chumba chenye giza.
Kuwa na furaha katika mwanzo wa maisha ni jambo jema, katikati ni bora na mwisho ni bora kabisa.
Cha mbayo wako hulishwa na mwema wako
Mali huzidisha furaha ya mwanamke katika maisha
Tunaishi katika dunia ya ajabu, hatumiliki vitu vyote, wala hatukosi vyote.
‘nchi ya usahalifu – usingizi’
Mwivu hatoshwi na nafasi, hata katika jangwa hataka kupishwa njia
Upotevu wa mtoto, hufufua tabu ya malezi kwa baba na hurudisha uchungu wa uzazi kwa mama
Friday, August 7, 2009
chacha wa Musoma on reach dad poor...
Although we have been successful in our careers, they have not turned out quite as weexpected. We both have changed positions several times-for all the right reasons-butthere are no pension plans vesting on our behalf. Our retirement funds are growingonly through our individual contributions.Michael and I have a wonderful marriage with three great children. As I write this, twoare in college and one is just beginning high school. We have spent a fortune makingsure our children have received the best education available.One day in 1996, one of my children came home disillusioned with school. He wasbored and tired of studying. "Why should I put time into studying subjects I will neveruse in real life?" he protested.Without thinking, I responded, "Because if you don't get good grades, you won't getinto college.""Regardless of whether I go to college," he replied, "I'm going to be rich."en looking for."
Tuesday, August 4, 2009
Hivi kwani nini watu huoga?

“
“Nimesikia habari za kusikitisha
Hizi ni nukuu mbili zilizonijaa kichwani kwangu. Ni siku ya jana niliporudi nyumbani mapema si unajua mambo ya foleni? Jana niliwahi ili nipate wasaa wa kupumzika na kutahajudi vya kutosha. Nilipofika home nikajikuta nikielekea bafuni.
Baada ya kuchojoa nguo zoote na kubaki uchi mzee mwenye ndevu akininginia, nikajiuliza hivi kwa nini niko hapa? Kwa nini niko uchi? Yaani nashika maji najirushia harafu nachukua sabuni na kujipaka, ili iweje? Ehe? Basi bwana nikaanza kufanya kile niaminicho ni kujisafisha mwili. Sasa mbona siwezi kutoka uchi mbele yako na mbele yaw engine lakini kwa ujinga najifungia mbele ya wadudu, maji na uchafu lukuki, nabaki uchi wakati wewe nakukimbia?
Kama maji dili mbona inyeshapo mvua huwa nachukua mwavuli au nakimbia
Sasa kwa nini tunaendeleza ujinga huu wa kuonga
Itaendelea...........
Basi nakumbuka nikiwa mdogo kule bush kwetu kuoga ilikuwa mara moja kwa mwezi au noma. Kufua nguo tulifua zile za shule tu. Nakumbuka baadhi yetu walipatwa na mabaka meusi kwenye ngozi japo hawakutoa harufu, life was always better,
Kuna nyakati shuleni walianza kukagua usafi, duh palikuwa hapatoshi. Ipo siku walipoanza kukagua usafi, mzee mzima nili tafuna kucha za vidole vyoote kumi ndani ya dakika moja kabla mwalimu hajanifikia kwani nilikuwa sijazikata wala nini. Washikaji walikuwa wanafuga chawa (enda) vichwani. Ipo siku mwalimu alikuagua vinywa
Monday, August 3, 2009
rich dad, poor dad
INTRODUCTION
There is a Need
Does school prepare children for the real world? "Study hard and getgood grades and you will find a high-paying job with great benefits,"my parents used to say. Their goal in life was to provide a collegeeducation for my older sister and me, so that we would have thegreatest chance for success in life. When T finally earned my diplomain 1976-graduating with honors, and near the top of my class, inaccounting from Florida State University-my parents had realized theirgoal. It was the crowning achievement of their lives. In accordancewith the "Master Plan," I was hired by a "Big 8" accounting firm, andI looked forward to a long career and retirement at an early age.My husband, Michael, followed a similar path. We both came fromhard-working families, of modest means but with strong work ethics.Michael also graduated with honors, but he did it twice: first as anengineer and then from law school. He was quickly recruited by aprestigious Washington, D.C., law firm that specialized in patent law,and his future seemed bright, career path well-defined and earlyretirement guaranteed.Although we have been successful in our careers, they have
Friday, July 31, 2009
kifo cha mzee Jasson Lutabasibwa kamala.
basi nikamkuta mzee F.kabigiza akiwa na piki piki cd fulani hivi. nilipomsalimia, mzee kabigiza hakujibu lolote, mzee kabigiza akaniambia kwa kihaya kuwa nahitajika Nyumbani kwetu. sikuuliza swali ila nilimwona headmaster akiniangalia kwa uzuni kubwa mno. nikawa kama nimechanganyikiwa na kuondoka mbiyo mpaka bwenini na kuchukua nguo mbili tatu.
nikiwa nimebebwa juu ya pikipiki, roho yangu haikuwa na amani na baada ya mwendo fulani nilisikia homa kubwa nikakaa kimya. tulipofika Bukoba mjini, kote nilikopita nikiwa kwenye piki piki niliangaliwa kwa uzuni na wale walionifahamu. twakaribia Nyumbani, mzee kabigiza akapunguza mwendo na kuniambia kuwa mzee amefariki jana yake. bado ilikuwa butwaa pia.
kufika eneo la kashura tulipokuwa tukiishi, nikaona watu wengi na hasa wale wa dini wanaimba nyimbo za kuommboleza, machozi yakanitoka, nikalia na kutamani kukaa chini. shangazi yangu akanishika na kunipeleka ndani, nikakuta mzee yumo ndani ya sanduku, ilikuwa ni kilio na kusaga meno.
tukasafirisha kwenda kijijini na kesho yake tukazika. maisha yakawa kama vile niko porini, kijana mdogo naachwa na dingi kumbuka sikuwahi kulelewa na mama wala simjui. duh niende wapi mimi mkosaji nisiye nazuri. yataisha tu lakini. tukamzika mzee wangu, nikabaki kuangalia kaburi na kulia, mara kadhaa nilikimbilia pale na kuongea na baba asiyeonekana!
baada ya kujitambua siku hizi nikagudua kumbe ni mambo ya kawaida na mzee ilibidi aondoke tu kwani isingekuwa hivyo asingeondoka. sasa nimezoea na nachuklia siiimpo baada ya miaka lukuki japo enzi zile nililia na kusaga meno japo hayakuisha. sasa ni miaka 11 na mimi ni jibaba na maisha ni meeema sana na namshukulu mzee wangu kwa upendo na kunizaa japo sikuliomba hilo.
kifo cha mzee kilinisaidia kumuona mama kwani baada ya kama mwezi mmoja hivi, mama alikuja kunitembelea shuleni, nikaitwa na na kumwona mwanamke aliyenizaa pale shuleni. hata hivyo alikaa kama dakika kumi na kuondoka kwa hiyo sikuweza hata kuikariri sura yake lakini nilifurahi mmno. mwaka wa 2001 nikaja dar es salaa na kumwona rasimi japo kwa siri au kwa kujificha.
duh sikuamini kumwona mwanamke aliyenizaa, nilijisikia kuwa mbinguni vile. nilimwangalia tumboni nilipoanzia maisha na kusema duh! japo sikukaa naye sana kwani ilibidi niwahi home na nilienda pale kisirisiri ili isiwe noma japo duh mama ndo hivyo. life is a process bwana na tumetokea kwingi na tunafanya mengi.
mpendwa msomaji wa blogu hii usione nakuzingua na mambo binafsi bwana kwani ni mambo ambayo nikishea na wewe najisikia vyema kwani wakushea naye ni kama sina vile! sijui niseme alazwe mahala pemo peponi mzee japo kutoka kwenye miili (KUFA) ni kawaida, muhimu na nilazima tu na sasa ni mambo ya kawaida kwa sasa.
Thursday, July 30, 2009
Ni ‘birthday’ yangu jamani.
Ni tarehe 30 July miaka 28 iliyopita ndipo kifaa nilipokatiza njia na kujitumbukiza ndani ya ulimwengu huu na kuwa binadamu mpya. Japo naamini kuwa niliwahikuishi sehemu, sijawweza kukumbuka ni wapi kabla ya kuuvua mwili (kufa) na kuuvaa mwili huu mpya tena nikiwa mhaya wa bugandika Bukoba mkoani kagera.
Tarehe 12/12/1982, nilibatizwa rasmi bila ridhaa yangu na kuwa mkrsto mfuasi wa uluteri ambao mpaka leo sijaweza kuuelewa wala malengo yake na hivyo nakaitwa James, Lutatinisibwa japo hivi sasa jina la james silitaki na silitambui tena na linikome kabisaa kwani sijui maana yaki ninini mimi na kwahiyo naitwa Kamala Lutatinisibwa
nikiwa kidato cha pili, toto hilooo!
Mwishoni mwa miaka ya 1980 nikaanza vidudu a.k.a chekechea za dini. Nakumbuka nilivyochapwa saaana ili niingie darasani kwani siku nyingine niliishia tu njiani na kurudi home. Nilipokuwa darasa la tatu, nikasomeshwa kipaimara na kuanza kula mkate kanisani wao wanaita kushiriki meza takatifu ambayo mpaka sasa nahoji utakatifu wake
Kuna wakati nilipenda mambo ya dini na kutaka kusomea uchungaji lakini ilikuwa ni kihere here baadaye nikabadirisha njia kwani utakatifu woote unaosemwa mimi naufanya bili kivuli cha dini wala unafiki wa kujificha mkuu. Kweli kwangu ni daima na unafiki ni mwiko!
Basi bwana, nilisoma vitu lukuki mpaka sasa kitaaluma ni mambo ya Compyuta nayo ni kwa kiherehere siifagilii wala nini ndio maana napenda kuandika na kuishi
Maisha yangu ya udogoni yalikuwa ni meema sana ili sikuwahi kufurahia upendo wa mama kwani inasemekana baba na mama walitengana mwaka mmoja tu baada ya mimi kuzaliwa (kumbuka ni mtoto wa mwisho) na hivyo nikalelewa na bibi yangu (ma yuliyana) na shangazi zangu kadhaa na binamuz.
Maisha yalikuwa mazuri japo mara nyingi ilikuwa ni kukwidwa na kuambiwa maneno fulani ambayo ni duh! I still miss something mother wise, am not yet mothered.
Mpaka sasa naishi maisha
Hata hivyo namshukuru kila mmoja aliyesababisha maisha yangu kuwa
Mabaya hukumbukwa na hivyo nakumbuka saana matusi na masimango yoote niliyorushiwa kwani wakati mwingine nikiyakumbukia hujisikia kulia kidoogo hata
Shukrani maalamu zimwendee binamu yangu Jennifer Lukambuzi, upendo wake kwangu
My sister Julieth, bro japhet nafwagilia kuwa na ndugu
Kila aliyefanya maisha yangu kuwa hivi, nampenda na kumfagilia na nashukuru kila mmoja aliyefanya kila juhudi kwa moyo ili kunitakia mema hata kama mimi sikulijua
Hata aliyelazimika kunisaidia ili jamiii imwone mwema naye namshukuru pia. Its my birthday, thanks to my beloved Vaileth for reminding me of this special day for she woke up yesternight and screemed; Happy birthday, happy birthday my love! Thanks and I appreciate to be with u.
Santamat spiritual master and fellow initiates, what a grace to realize my higher self? We shall never die but merge back to be one with HIM, thanks to sant Baljit Singh and all past masters!
hapa nshajua kuruka juuuuuuu na kucheza, 2002, moshi
Tuesday, July 28, 2009
darasa lilikuwa hivi kama lionekanavyo
kwa kifupi nilitoa mada juu ya haya yaonekanayo ubaoni, it was nice, I wish more blogu will be created, bofya hapa kuona moja wapo iliyotengenewzwa
Friday, July 24, 2009
uandish wa kiraia
Wednesday, July 22, 2009
Monday, July 20, 2009
Swali kwa wenye Blogu
ni chamgamoto gani unazipata katika blogu? je unadhani blogu zinaweza vp kutuletea mafanikio na maendeleo endelevu? ni matumizi gani mengine ya blou unadhani ni muhimu? je maisha yako yangekuwaje sasa bila blogu?
unadhani kuna umuhimu wa jamii zetu kuwa na blogu? unasemaje juu ya taarifa na uhuru uliyomo kwenye blogu? kuna umhuhimu wa kufundisha watu wengine na hsa vijana kuwa na blogu na kuwawezesha kutembelea blogu nyinginezo?
natanguliza shukurani.
Friday, July 17, 2009
nawapenda sana wanawake na ma Jike pia
ukisema au ukisikia wanasema jamaa anapenda sana wanawake, waelewa kuwa anapenda zaidi labda ''kusini mwa Afrika'' mimi nafagilia kila kiumbe cha kike, wanasema wanawake ni wadhaifu, kumbe sio, bali ni walaini. kwa sababu yao, ndiyo maana ulimwengu unazidi kuwepo. kwa sababu ya uwepo wa viumbe wengine wa kike ndio maana ulimwengu unazidi kuwa na viumbe hivyo. uanaume wangu, unajidhihirisha ndani ya mwanamke. ni kwa kumpataia mbegu, ndipo anazaliwa mtoto wa kuniita baba. ni mwanamke. upendo wa mama sio wa kawaida kwa wanae, atafanya kila awezalo kumlinda mwanae. Mwanamke anatumbo la ajabu, ni tumbo linalotunza na kuzaa viumbe vingine. tunamla mwanamke kwa kunyonya maziwa yake na kwa hiyo mwili wake ndio chakula chetu. mwanamke sauti yake ni nzuri, sauti yake ni njema sio ya kibesi wala nini. NAMPENDA mwanamke. lakini unaweza kuamini kuwa tangu nizaliwe sijawahi kuunja upendo wa mama wala wa Mwanamke yeyote?? nakosa mengi ndugu, sikuwahi kuuonja upendo wa kweli japo natambuaumuhimu wa mwanamke. aaaamina
huwa mnafikiria nini?

wengi wenu mkiingiaga kwenye mijengo kama hii huwa mnakuwa wanafiki wa kujifanya wanyenyekevu na wenye upendo, wapole, wasiopenda kuzini nk.
kumbe waongo mnaogopa ule mkwala mkuu upigwao wa siku za mwisho takutana na limoto la milele likuunguze mpaka kinyesi kilicomo tumbona mwako.
nawakemea. Mkasali bwana
Thursday, July 16, 2009
mmmmhhhhh nnnooooooot! unaona nini?
labda hata sungura wanazunguka,tafadhali blogu hii irudi kwenye maadili sio vitu vya gizani please, ombi!
Wednesday, July 15, 2009
Kila kitu kinazunguka.!
Wanasayansi wanatwambia kuwa ulimwengu / dunia tuishimo ni duara na kwamba inazunguka jua. Mzee mmoja kule kwetu anabishi kwamba dunia imetulia ila jua ndo lenye kiherehere linazunguka dunia. Kwake dunia ni kubwa kukliko jua.
Basi nyota nazo zinazunguka, mwezi nao mala kipande, mala mzima. Wengine wanasema macho yetu ndiyo yaonayo mviringo.
Basi bwana, maji tunayokunywa yanazunguka. Yanatoka mitoni, baharini au kwenye madimbwi kwa kuakisiwa au kuchavushwa na baadaye kunyesha kama mvua. Hata mikojo, vinyesi na mate, yanaakisiwa na kunyesha kama mvua harafu wewe unakunywa. Yawezekana maji unywayo sasa ni mkoja au mimate ya lijamaa usilolipenda!!
Chakula nacho ndo hivyo. Ukijisaidia shambani yanaota mazao mazuri yenye mbolea na matamu kula, yanazunguka. Binadamu naye anazunguka, tuachane na reincarnation, unatoka hapa na pale huku na huku kule na kule. Damu inazunguka mwilini na ikisimama hamna uhai!!
Akili zetu nazo ziko bize, mara hiki, mara kile, mara sijui nini. Mchana mawazo, usiku ndoto, zikisimama wafa. Kila kitu ni mzunguko tu. Basi kama kuna herufi nzuri, ni O au 0 kwani zinaonyesha uhalisi. Ni mzunguko tu ndg.
Nini kingine kizugukacho? Si hata gari lazima lizunguke ili kukufikisha uelekeako?
ZUNGUKA TU
Monday, July 13, 2009
unamtafuta Mungu? acha hizo!
Hatuwezi kumjua Mungu na hivyo tunachokijua ni kama punje ya mchanga baharini. Mungu hayuko mbali nasi. Hatuwezi kumtafuta huku au kule, tunaweza kumpata kwa njia ya uamsho pekee, uamsho (awakening) wa roho zetu. Roho pekee ndiyo inayoweza kumwona Mungu. Ndio maana wanasayansi hukataa juu ya uwepo wa Mungu hata kama ukubali juu ya uwepo wa nguvu wasiyoielewa inayomiliki na kutawala kila kitu..
Uamsho wa roho zetu huanza kwa kujitambua. Ukijitambua utamtambua Mungu. Uamsho wa roho ni sawa na sayansi ya roho, sayansi iwezeshayo kumuona Mungu. Kwa uamsho wa roho zetu, tutamhishi na kumfurahia Mungu. Roho ina kazi maarumu ambayo ni kumhisi, kumjua na kufurahia baraka za Mungu.
Vitabu vya dini (misaafu) husisitiza kuwa sisi ni roho na kama ni roho sisi hatuna mwanzo wala mwisho na sisi na Mungu ni sawa na maji. Mungu ni mkubwa kama bahari na sisi ni wadogo kama tone la mvua na hivyo basi tone la nvua lidondokapo baharini huwezi tena kuyatenganisha. Bahari hupokea maji ya kutoka kila upande kama ishara ya umoja wa binadamu wote wenye rangi, kabila na mataifa tofauti. Bahari hupokea maji kutoka bara ulaya, Amerika, Afrika na kwingineko lakini maji yale yaingiapo baharini huwa kitu kimoja. Rangi moja, radha moja na sifa zilezile. Huwezi kuyatenganisha tena kwa kuangalia yalipotoka. Hivyo ndivyo ilivyo kwetu sisi kama roho tukifika mbele ya Mungu huwa kitu kimoja
Vitabu vya dini pia huongelea juu ya nuru na sauti (neno). Mungu yumo ndani mwetu na nilazima tumjue huyo wa ndani kabla ya kumtafuta wa nje yetu kwani tukimhishi ndani mwetu tutapata Muunganisho naye (kwanjia ya roho) na hivyo sisi na yeye kuwa wamoja kama ulivyo ukweli mkuu. (kumbuka sisi ni sehemu ya ukweli mkuu au ukweli mkuu umo ndani mwetu)
Thursday, July 9, 2009
Njia ya kuelekea kwa Mungu
Kutoa huduma kwa wengine bila kujigamba na kuheshimu kila kiumbe chake kuazia kwa binadamu, wanyama miti nk.
Kukumbuka na kulinuiza jina lake na upendo wake wakati wote (tahajudi ya nuru / inner-light meditation).
Kusikiliza maneno yake na sauti yake kupitia kwa viumbe vyake (tahajudi ya sauti / inner-sound meditation)
Na kuishi kwa uwepo (kuishi sasa / consiousness)
Haya yote yatatuelekeza kuishi kwa upendo, amani, mafanikio vitakavyo zaa heshima, umoja, kuvumiliana, heshima na kutupelekea kwenye uhalisia wetu (ukweli mkuu) ambao inasemwa kuwa mkiijua kweli itawaweka huru na hakuna uhuru bila kujitambua (self realization) ili kumtambua Mungu (God realization)
Kristo (yesu) anatwambia kuwa kama mnanipenda, basi ziiishi amri zangu
Tuesday, July 7, 2009
njoo darasani tujitambue wewe!
Familia ya Jitambue (FAJI) ni Umoja wa Wananchi wa Tanzania wanaojishughulisha na maarifa ya utambuzi. FAJI ni Taasisi iliyosajiliwa Mwaka 2007 yenye namba ya Usajili 15579 chini ya Msajili wa Jumuiya, Wizara ya Mambo ya Ndani.
Utambuzi ni maarifa yanayolenga kumuwezesha mtu kubaini kuhusu yeye na yanayomzunguka ili aweze kukua, Kimwili, Kiakili, Kihisia na Kiroho. Kwa kuyapata maarifa hayo yanamuwezesha kuachana na mazoea yanayomuumiza na kuumiza wengine; kukabiliana na vikwazo, vurugu na changamoto mbalimbali za kimaisha; kufikiri vizuri, kujiamini, kuwa mbunifu, kufikia malengo yake na hivyo kujiletea mabadiliko katika maisha yake na maendeleo ya jamii kwa ujumla. Pia humfanya mtu awe na ufahamu yakinifu wa ubinadamu wake na hivyo kuweza kuishi maisha yenye Furaha, Amani, Utulivu na Upendo wa kweli. Kujifunza maarifa hayo huhitaji kuwa na sifa yoyote maalumu kama cheti cha shule, umri, jinsia, dini, imani nk. Kitu kikubwa ni uwezo wako wa kuyatekeleza unayojifunza kwa vitendo.
Kwa sasa FAJI inajishughulisha kusambaza maarifa hayo kupitia vyombo mbalimbali vya habari pamoja na Madarasa yaliyopo kwenye Kituo cha FAJI Kimara Rombo Dar es Salaam.
Maarifa haya pia yanatolewa kwa njia ya Semina kwenye Shule, Vyuo, Taasisi na Mashirika mbalimbali.
Baadhi ya mada zinazofundishwa ni:-
Namna ya kupata utajiri pamoja na mafanikio katika biashara, kiuchumi, kazini na shuleni; namna ya kujenga mahusiano mema kazini na upendo wa kweli katika ndoa, suluhu ya tendo la ndoa; namna ya kujiamini; kuondoa msongo wa mawazo, chuki, kijicho na hasira za ziada; kinga ya uchawi; namna ya kupata chochote utakacho maishani; kuondoa tabia sugu kama ulevi, uvutaji sigara n.k., kuondoa hofu na aibu, kupata afya nzuri kimwili kwa njia ya tiba mbadala, kufikiri vizuri, n.k.
Tunafundisha mada nyingi zaidi ya zilizotajwa hapo juu.
Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nasi kupitia:
Sanduku la barua namba 22040 Dar es Salaam. Simu namba 0652 626996, 0715 627003 au 0784771301 na 0713 250701, Email – faji.jopo@gmail.com au fika katika kituo cha FAJI kilichopo barabara ya Morogoro Kimara Rombo na utaliaona Jengo la Taasisi ya FAJI kulia kwako ukiwa unatokea Ubungo.
wakazi wa Mwanza darasalitakuwepo kabla mwaka huu haujamalizika, jiandikishe kwangu kupitia 0754 771 601
Monday, July 6, 2009
wajasiliamali wa bongo wanaigana!
ubunifu ni mdogo sana. yaani mtu anashindwa hata kuogeza vikolombweizo na kuwa na tofauti na mwenzie, kila bidhaa ni zile zile. kwa maneno mengine ukitembelea banda moja la wajasiliamali wa bongo huhitaji wenda kwingine kwani unakuwa umeona kila kitu ambacho labda ungekiona kwingine! duh
mimi ni mpenzi wa nguo za kiafrika, hakuna jipya! nguo zote zinafanana. nilipowatembelea wakenye, kidogo nikaona utafouti na mvuto. sikupiga picha labda ningekushirikisha kwa picha ukaona. ni lini wajasiliamali watakuwa wabunifu na kushindana vyema? mimi sijui na labda sitaki kujua saana.
ndo hayo
Thursday, July 2, 2009
Tumesahau na kuacha kazi iliyotuleta duniani.
makala haya niliwahi kuyaandika katika jarida la rai.......
Binadamu kama viumbe vingine kaletwa duniani kwa sababu maalum ili kukamilisha kazi maalumu ambayo maumbile (Mungu?) yalimtuma kuja kuifanya hapa duniani. Ndio maana kuna watu wenye vipawa na uwezo tofauti tofauti katika mazingira yetu tunayoyaishi. Kila mtu katumwa kuja kuitenda kazi fulani na akiimaliza, arudi au aondoke.
Wengi tumepotea na kupotoka na kuingia kwenye vitu vingine. Tumevamia kazi za wengine na kuishi kwa kuongozwa na tamaa kwa kuvutiwa zaidi na anasa za dunia hii. Mwili wetu wa hisia kwa kushirikiana na akili zilizojazwa mawazo hasi kuliko yale ya chanya, ndio umekuwa kiongozi wetu. Tunapenda kujionyesha, kujisifu, kujisikia na hivyo tunatawaliwa na matatizo ya kihaiba (ego) zaidi kuliko uhalisia wetu.
Mtoto akishinda mtihani au akipelekwa shuleni, haruhusiwi kusomea kile anachokipenda bali hulazimishwa na wazazi kusomea kile kilichowashinda wao au chenye sifa ili waje kujisifu jinsi walivyokuwa na kijana msomi wa fani fulani nzuri hata kama yeye haipendi na hivyo kumpotezea lengo lake la kutimiza kile kilichomleta duniani kufanya.
Maisha yetu yanazidi kuwa ya hovyo yasiyo na msimamo wala mwelekeo, ni bora liende tu kama vile tulikuja duniani kwa bahati mbaya vile!
Wanasiasa na viongozi mbali mbali wapo kwenye nafasi walizonazo ili wapate wao mradi au kwa sababu kunalipa japo yawezekana hawapendi kufanya kazi wanazozifanya. Hata wewe unayesoma hapa yawezekana hupendi kazi yako, unaifanya basi tu kwa sababu ulilazimika kuisomea au upate pesa. Hakuna binadamu aliyekuja duniani kutafuta pesa bali pesa ni matokeo ya kufanya vyema kazi zetu na hasa zilizotuleta.
Ndio maana tunaishi na jamii yenye uchungu, visasi na hasira kwa sababu kila mtu anachukia kila hali na mazingira ya kazi yake kwa sababu hakupaswa kufanya kazi hizo.
Ukichukia kazi yako kwa kujua au kwa kutokujua, basi ujue unajichukia wewe mwenyewe na huwezi kujipenda. Ndio maana wanasiasa wanajiongezea pesa na wengine kukumbwa na kashifa kibao za rushwa, ni kwa sababu waliingia kwenye kazi hizo kwa tamaa ya fedha na sio kwa upendo wao au kazi zilizowaleta duniani.
Wazee wetu wakizeeka tunawatafutia vijikazi ili wazeekee pale, je unategemea ufanisi hapa ua kuboronga kama tunavyoona? Sasa tunakaa penmbeni hata majukumu yetu tunawalaumu wengine kwa kutokuyatimiliza. Tunategemea misaada kutoka kwa wahisani na tunailalamikia serikali na kuitukana utadhani sio serikali yetu kumbe suruhuisho la matatizo yetu yamo ndani mwetu!
Hatuna budi kujikagua na kutafuta ni wapi tulipoteleza na kurekebisha mara moja. Yatubidi kudadisi na kujua kazi zilizotuleta duniani ili tuishi vyema kwa furaha na kwa faida ya jamii pana. Ndio maana wasanii wa miziki ya kizazi kipya wanaimba nyimbo za kimapenzi tu. Kwa sababu wao hawajazaliwa kuimba hata kama wanasauti nzuri na hivyo wanaimba tu kwa sababu wamepata nafasi ya kuimba. Waigizaji wa filamu nao hawana jipya. Ukiangalia filamu zao hazifanani na mazingira ya ‘Bongo’ na hivyo kuigiza sio kazi yao, ni kwa sababu wamejikuta huko au mazingira yamewalazimisha kuingia huko au hawana jinsi.
Tafuta kazi yako na uifanye vyema. Kazi yako ya kwanza iliyokuleta duniani ni malengo. Wanasema maisha ni malengo na kwa hiyo lazima ujiwekee malengo ya msingi na kuyafuata. Nasema malengo ya msingi kwani malengo mengine hayana maana. Kama lengo lako ni kujilimbikizia pesa au kupata utajiri mwingi basi iwe ni kwa kufanya mambo ya msingi na sio kupitia njia za panya kama kuingia madarakani kwa kununua kura nk kwani kufanya hivyo kutakusababishia matatizo ya shutuma, tuhuma, malalamiko na laana.
Basi lengo letu kubwa liwe ni kujua vipawa vyetu na kazi zilizotuleta duniani ili tuishi vyema na kwa furaha. Kumbuka kuwa lengo ni jambo lolote lile ambalo katika kulitimiza kwako unakuwa na furaha na kwa hiyo kama unataka pesa lakini unafanya kazi usiyoipenda, ni bora kuachana nayo na kufanya ile uipendayo ili uwe na ufanisi na ubunifu katika kazi yako.
Utajua kazi iliyokuleta kwa kuifanya, kuifikiria au kuona wengine wanaifanya. Ni kazi itakayokupatia furaha na ridhiko la kweli kila uifanyapo au uonapo wengine wanaifanya. Tusiogope sana vitisho vya dini zetu kwani dini zetu nyingi nazo zimevamiwa na watu ambao hawakupaswa kuziongoza na ndiyo maana vitisho vya kuingia motoni vinaongelewa zaidi kuliko uhakika, usalama na amani ya kuingia mbinguni (kiimani zaidi)
Niwakati wa kuitafuta na kuitumikia kazi iliyotuleta duniani. Sisi kama binadamu ni lazima tuwe na utu, upendo na amani ili tuweze kuheshimiana na kusaidiana vyema na kuishi maisha ya ukweli na uhalisia kuliko ya kufoji yenye mateso na lawama tele.
Ebu kila uamkapo asubuhi jipangie ni kazi gani utafanya na ni ipi unayoipenda na jioni kabla ya kulala angalia ni kwa kiasi gani umeitenda kazi hiyo na kujipongeza hata kama ujaimalizia kwa kujihaidi kuimaliza tena. Furaha ya kweliitaanzia hapo na malengo ya kweli na ya msingi utayatengeneza na hiyo itakuwa ni hatua nzuri ya kuwa na malengo nakubwa zaidi yatakayofanya kipato chako kuongezaka.
Tutafute sababu ya kuumbwa ketu na kuikamilisha. Tujenge moyo wa kujiamini kwani tukijidharau tutadharariwa ila tukijiamini, tutaaminika na kuishi vyema. Eti wewe ungependa ukishakufa (kwani ipo siku uataondoka tu) au ukiacha kazi yako au uwanasiasa wako, ukumbukwe kwa lipi? Tuhuma, uzembe, majungu unafiki au kusaidiana, heshima, umoja malengo nk? Kwa nini usikumbukwe kwa jambo zuri la kusaidia jamii? Unadhani akina Nyerere walifanya nini zaidi ya kuitumikia jamii kwa moyo, uadilifu, umoja na malengo?
Rudi kwenye kazi iliyokuleta duniani bwana.
Wednesday, July 1, 2009
umeoa / olewa?
|
Monday, June 29, 2009
unapolazimika kuficha kicwa, unaacha nguo......

Ukimfumania Nyani au ngedere shambani mwako badala ya kukimbia huwa anachukua vidole na kujificha uso akidhani humwoni kumba unaweza kumtungua utumbo ukumwagika woote nje! Duh
Kuna yule ndege maarufu akikuona anaficha kichwa mchangani na kuacha kiwiliwili nje akidhani kwa kuwa hukuoni basi na wewe humwoni na kwa hiyo utaendele kumbe anaogopa kufa anaona!
Sasa angalia huu ubunifu. Jamaa anaacha miguo yake michafu, anakimbia kuingia nyuma ya pazia kumbe kuna kijibwa chenye kiherehere. Imajini jamaa kaacha kila chake, harafu yuko mbele ya luteni Kanala ambaye kwa vyovyote ana mguu wa kuku! Duh sijui anafikiria nini hapa.
Walianza labda kwa kutaniana na kujikuwa sehemu za kusini kwa miili yao zinachekelea kwa misuguano na migogoro ya kelele zisizosemekana na kusahau kufunga mlango. Hapa wanatamani wasingejuana aka wanajuuuuuuta kujuana.
Je ungekuwa wewe mmoja wa hawa na hasa huyu nyuma ya pazia, ungefanyaji? Au iliwahi kukutokea? Unadhani ungekuwa hili lijamaa la manyota ungepata fundisho gani? Au ungepige mtu tu ili akukome?
Unataka kujua ningekuwa mimi ningefanyaje? Je huyo nyuma ya pazia akijulikana kuwa ni ndugu wa hili lenye manyota, au bosi wake au mwajiriwa wake, house boy je? Nini kiliendelea?
Mimi simo!
Friday, June 26, 2009
Michael Jackson alipata maumivu ya kihisia na kiakili akajikana

Nimesoma kwenye mtandao mmoja kwamba baba yake Jackson alipendendelea kumuita bignNose a.k.a puaKubwa. Bila shaka Jackson alibeba kichwani mwake kuwa pua lake ni libaya na labda ngozi yake ni mbaya na labda jinsia yake ni mbaya, nk nk. Hapo ndipo lilipotatizo la kutukana watoto wetu na kwa hiyo mike Jackson kujibadili rangi na kila kitu ilianzia kwa babake.
Mwalimu wangu wa maarifa ya utambuzi hayati Munga tehenan aliwahi kutembelewa na mtu mmoja akitaka ushauri kuwa afanya nini kwani alijiona mbaya na mwenye masikio mabaya saana. Munga akamwita mwanae aliyesoma darasa la saba wakati huo. Akamwambia amwangalie jamaa Yule kwa dakika kama mbili, na baadaye akamwambia unamwonaje? Motto akajibu ni mzuuri sana. Akamwuliza tena, na masikio yake Je? Mtoto akayaangalia masikio na kujibu ‘mbona mazuri sana kuliko hata ya kwako baba?’
Jamaa hakuamini, alipoulizwa kwanini alijiona vibaya, akajibu kuwa tangu azaliwe mamaye alikuwa akimtusi kuwa yeye ni mbaya, mjinga na hana akili. Mimasikio yake imekaa kama ya popo na matundu ya pua yake ni mabaaaya sana
Hivyo hivyo namdada mmoja alikuwa akitukanwa usukumani kwao kuwa ni mbaya. Akakutana na shangaziye jijini Dar, shangaziye akamsifia, kuwa ni mzuri, hakuamini na alipojalibu kuingia katika mashindano ya urembo na kupata nafasi ya juu. Yeye alijiona mbaya na kuambiwa kuwa wewe ni jinga na baya ni hatua ya kuizarau sipoweza kuziepuka.
Hata mimi ndugu msomaji, udogoni nilikuwa nikiambiwa kuwa mimi ni jeusi na baya kule shuleni. Jinga nyumbani na nina bichwa kubwa. Duh, kumbe sifai. Nilipoenda kusoma mjini moshi, nikashangaa na kujisikia vibaya kwani wacchaga (na hasa mabinti) walikuwa wakiniangalia kwa mshangao na kwa mud mrefu. Kwa hiyo kila niliposalimiana na mchaga kwa kusikana mikono, niliangalia rangi. Kono langu lilionekana jeusi kama mkaa mbele ya ule wa mchagga!
Duh nikaja kugundua baadaye kwamba kumbe wachaga walinipenda na walishangaa sana kuona rangi ya ngozi yangu. Kumbe hata kama ni mweusi, bado ninangozi nzuuri ya kuvutia nay a ajabu *(si unajua weusi wa kihaya) kumbe wachaga walinifuraia na kunipenda wakati nikijikana na kujiogopa. Ningekuwa Michael Jackson, ningejichubua kumbe najiharibu.
Hata wewe jikague, linganisha maneno uliyoambiwa udogoni na jinsi yanavyokuathiri saana maishani mwako, lakini pia kuwa makini na maneno unayowaambia watu na hasa watoto na wale walioko chini ya mamlaka yetu, yanaweza kuwaathiri maisha yao yoote na kujikuta tunawapoteza. Penda kuwa chanya a.k.a positive katika maneno na matendo uwatendeayo wengine, ni muhimusana. Mike aliharibiwa na baba yake bila baba kujua, kwa kumwita pua kubwa!
Thursday, June 25, 2009
Monday, June 22, 2009
Maisha yetu bongo na jamii yetu…
Bongo kuna shirika la TGNP, linapambana na matatizo ya kijinsia, kweli? Si mradi ule? Unadhani wanapenda kupunguza matatizo ya wanawake? Yakiisha watakula wapi? Angalia machapisho yao, mengi yameandikwa kwa kiingereza! Na picha zake zinaonyesha wale wanaopigwa na kunyanyaswa, hazionyeshi wale wanaoishi vyema na siri ya wema huo ili kiwe chanzo cha mabadiliko!
Kwenye mikutano yao wanawajaza hasira wamama! Hivi mtu ambaye hajajitambua anaweza kweli kushinda matatizo ya kijisinsia? Shirika la kupigania wamama wa Tanzania linatoa machapisho kwa kizungu. Lipo mtandaoni, linajulikana kwa wato wa nje (watoa pesa aka donors kuliko walengwa). Machapisho ndo hivyo ya kizungu kwani si donor anajua kizungu?
Wanaonesha matatizo na sababu ya kuendelea kupewa pesa badala ya kumaliza tatizo. Liishe ili? Kila mtu ni mradi. Wajanja wanatumia matatizo yawengine kuwa miradi kuna mashirika kibao ya vijana, wafungwa, wazee, wagonjwa nk.
Yanajulikana zaidi kwa wenye fedha kuliko walengwa. DUH inatisha, wajanja wameshatufanya miradi yao, wanafanikiwa pia. Ni maisha ya Bongo. Kila kitu kina milikiwa na kina wenye nacho.
Tamaa zatuongoza. Kila mtu anatamani mke, wake waume nyumba, magari nk. Bongo ni kulewa na kukimbizana. Sisi ni masikini, hatuna kitu. Tunalia tunajiendea tu
Vijana wanatafuta nafasi za kwenda nje kusoma, na kufanya utumwa, wanaita green pastures! Ni maisha ya bongo, watoto wa mitaani wanaongezeka, wanajilea, wanapigwa tu. Hupigwa na jua, mvua, baridi, joto, mawe, wapiti njia na hata miti. Hawajawahi kupendwa, hawajui kupendwa, wakiwa wakubwa itakuwaje? Ni bora ufe wapate sh 500 kuliko kuishi wakaikosa.
Ni maisha ya bongo, ni utanda wazi, ni diri za miradi! Kila mtu sasa diri. Kuna mradi unaokufanana unaendelea. Vijana wanaamini kutika imani za ajabu kupata utajiri. Dini zipo na vitisho zinavyojua kupeleka watu mbinguni wakati duh? Tungekuwa na dini matatizo yangeongezeka hivi?
Bongo, bOngo, boNgo, bonGo, bongO ni maisha ya BONGO ndani ya ugiligili na ubeuzi
Sunday, June 21, 2009
maisha ya Bongo.... --4
sasa tuangalia juu ya kinachoitwa vita ya kijinsia. eti mwanamke ananyanyaswa na kuna watu wanapigania kinachoitwa haki sawa, eti kumtetea mwanamke asinyanyaswem wanataka mwanamke awe kama mwanamume, naye afanye kazi kama afanyazo mwanamume.
unaweza kujiuliza bila jibu kuwa; haki za mwanamke ni kuwa kama mwanamume au zimeshikiliwa na huyo mwanamume? sasa mambo yamebadilika, mwanamke anafanya kazi kufukuzia ela ili aheshimiwe na mwanaume hivyo hivyo, watoto wanajilea kupitia house girl kwa kusaidiana na TV, ndo hilo taifa la hovyo linajengwa
vita ya kijinsia inapamba moto, mitandao kama TGNP inaangahika kutetea haki za wanawake, inawashauri waachane na mijianaume ya hovyo, mama anatii, unakuwa mwanzo wa watoto wasio na baba wala wazazi,. baada ya kutoka kwenye ndoa, mwanamke anagundua sio suruhu ya matatizo, anatamani kurudi, Mume alishaoa tena, ni matatizo juu ya matatizo kumbe yawezekana tatizo sio mwanaume.
tunaishi tu, tumeoana bila elimu yoyote juu ya ndoa wala tendo la ngono. mambo ni hovyo, haielewiki hatuelewani. maisha ya bongo yamejaa simanzi na majuto ya hapa na pale. tunajiendea hovyo. fumanizi ni nyingi. watu wanajaribu kuonja radha tofuti, kumbe si suruhu pia. ni ndoa Bongo ni maisha ya vijana wa bongo; yamepoteza maana, yamepoteza uhalisia, ni hovyo, ni vurugu kwa kwenda mbele!
Friday, June 19, 2009
maisha ya Bongo, vijana wa bongo maisha yetu duh-3

Wednesday, June 17, 2009
maisha ya Bongo, vijana wa Bongo - 2

naendelea kuyaangazia maisha ya wabongo na ya vijana wa Bongo
maisha ya vijana wa bongo walioko mashuleni na vyuoni ndo mawee? ukimuuliza kijana anayesoma kuwa anapenda kusomea nini atakwambia kozi yoyote au kozi fulani kama vilie uhasibu. ukimuuliza kwa nini uhasibu atakwambia kuwa una ajira nyingi> duh ikiwa na maana kuwa yeye alikuja duniani kufuanya chochote au kutafuta pesa ili ale anywe ashibe na afanye ngono!
kacha! akimaliza shule ajira ndo hivyo, anakaa kijiweni, maisha ya shule ndo hivyo, hayakuwa na muelekeo. alifukuzwa, alikula mlo mmoja nk. akiingia kazini sasa basi, ni pesa, ni rushwa ni lawama. atatembelea viwanja vyote as if duh, aliishi ili vimkome. ukimpa uongozi ndo rushwa tu si alisomea msosi?
kijana anatanga tanga mitaani, akikutana na wanaofanya kazi wanamtishia na kumpiga mkwara kuwa hakuna kazi au akushinda vizuri. kijana msomi wa bongo sio mbunifu, anatafuta ajira! kah! inauma!!!! yupo yupo. anatamani gari, ndoa na maisha yoyote. ni mlevi, mulokole na ni mbahatishaji.!
kanicosha kijana wa bongo, mawazo yake duh
Tuesday, June 16, 2009
maisha ya Bongo, vijana wa bongo maisha yetu duh-1

Monday, June 15, 2009
mipira yetu, ngumi na haira badala ya raha


ndg,
angalia hizo picha mbili, majamaa wanasaidiana kuruka ukuta ili wakaangalie mpira, harafu wakiisha kuwa ndani basi ni ubabe kwa kwenda mbele. sasa angalia hiyo picha ya chini mijamaa inapimana nguvu.
udogoni nilishabikia saana mpira. mpaka nakuwa kijana niliitwa Jonas Lunyamila (jina la mchezaji wa yanga) na baadaye nikaitwa davd becham kwa sababu nilicheza namba saba. nashangaa kwanini nilioewa majina wa wachezaji wakubwa namna hiyo wakati mpira ulikuwa haupandi! nilikuwa nikiingia uwanjani dakika za mwisho au kujaza tu pengo!
ningeweza kujifunga au kuacha mpira nikakimbia mbiyoooo kama vile nina mpira! duh, asikwambie mtu.
basi ukubwani nilipunguza hiyo hamu ya mpira. miaka yoote niliyokaa Dar sijawahi kuingia uwanja wa Taifa zaidi ya kupita kwa nje nielekeapo mbagara rangi tatu. kilichonikatisha tamaa ni baada ya kusikia story za kutisha kuhusu utazamaji.
eti ukikaa upande wa simba, yanga ikafunga ukashangilia, unatwangwa mkanda! mara majamaa wanakujoa kwenye chupa ya maji na kukurushia! duh mara nini. sasa angalia hao wanavyokamatana mashati
Saturday, June 13, 2009
Thursday, June 11, 2009
Turudi kwa wakristo na msalaba.
Unajua toka nikiwa mdogo ilipenda sana utafiti. Na ndio maana ninablog kwani inanisaidia kujua mengi na kuwajulisha mengi wengine. Udogoni nilipouliza maswali ya kutaka kujua zaidi hasa juu ya dini nilikwidwa. Kwa mfano kuna siku tulienda kanisani kumwomba mungu atulinde dhidi ya wezi wa usiku, kesho yake kanisa tuliliosalia likavyunjwa na kuibwa viyoo na milango, nilipouliza juu ya huyu mungu asiyelinda kanisa atatulindaje sisi? Nikajibiwa eh? Unasemaje
Nikadhani sikueleweka nikauliza tena, mbona kanisa tusaliamo limeibiwa sasa tutakuwaje na usalama?
We!! Nilisikia kofi nikadhani ni muujiza na lundo la fimbo, kisa? Nimekufuru na nisipotubu nitaenda motoni. Ningekuwa nimepata kipaimara basi ningezuiwa kushiriki mpaka chini ya marudi, we?
Tuyaache hayo. Swali langu la wakristo kuutukuza msala na kuufanyia biashara limepanuka na labda kujibiwa. Gazeti moja linaonyesha ushahidi kuwa hapo kale warumi walinyanyasa watu na kuwatundika kwenye mti imara ulionyooka na sio msalaba. Linasema msalaba ni ishara ya kumtukuza Mungu wa uzazi wa enzi za mababiloni na sio kweli kuwa alitundikwa Yesu bali yesu alitundikwa kwenye mti mmoja ulioonyooka kwani wanasema biblia ya kigiriki inasema tauros likinaanisha mti mmoja na sio msalaba kama tudanganywavyo
Linauliza swali juu ya kuutukuza msalaba kuwa kama nduguyo kapigwa na rungu kichwani na kufa, utapenda kuchukua rungu hiyo kama ukumbusho? Je utaiigiriza na kutoa nyingine kama hizo na kuwsambazia nduguzo wote ili muutuze kama ukumbusho wa hasira na kifo au mtautupilia mbali kupunguza hisia kali?
Ukiangalia siku hizi misalaba ni dili namingine ni ya dhahabu na bei juu. Mingine inauzwa bei kali na inaabudiwa kuliko hata Yesu mwenyewe namafundisho yake, je wewe unafikiri vipi juu ya Mungu wa kibabiloni na alama zake? sijiui
Wednesday, June 10, 2009
nyimbo hii nazo
Sikiri mimi masikini uvivu wangu nyumbaani,
ukiwa huunjiana nakufa hapa kwa nini
sadiki sasa ashiiba chakula kingi kwa baba
nirudi tena kwa baba nakufa hapa kwa nini
naombaradhi nimekoosa ntakuwa mtoto mwema sasa
nitakuwa kama sadiki
na nyumbani tena sitooki baba na mamanisameeni
twapenda mambo yoote ya shule kabisa
kujua kusooomatwaona furaha
hhhA hhhE hhhI hhhO hhhU
twaimbavyema leo..
ongeza nyinine basi na wewe. hii inaitwa short break
Monday, June 8, 2009
furaha nini na iko wapi?
katika ulimwengu huu tunaoishi, mwanadamu amehangahika na anaendelea kuhangahika akaiitafuta furaha, amani na upendo wa kweli. katika hilo, kwa kutumia akili zake, binadamu ameishia kutengeneza matatiizo lukuki yasiyoongeleka.
je wewe unajua furaha ni nini na inapatikana wapi? amani ya kweli na upendo je?
tunafananisha furaha na vitu vya duniani kama vile fedha, utajiri, majumba magari nk, lakini wenyenavyo nao hawana furaha wala amani. wanajifungia jera kwa kulinda mali zao hizo. je furaha ya kweli iko wapi sasa? na mamani je?
hata kwenye nyumba za ibada ni vita. mitaani mamamaa, baa duh. elimu ndo maweee, utawala wakisiasa nk. wengine wamekuwa wachawi, ulevi nao ndo hhuo lakini mwisho wa yote nimateso.
waafrika tunatafuta utajiri japo nchi tajiri watu wanaongoza kwa kujiua kisa? hawaoni maana ya maishi hata kwa kuzunguwa na utajiri. je waafrika tunaishi maisha yenye maana zaidi? furaha inakaa wapi lakini?
Obama anatafuta amani ya dunia huku akiwa na siraha kali na jeshi kubwa, kamwe hawezi kuipata. tumeshindwa kujua kuwa furaha na amani ya kweli vimo ndani mwetu. tunasahau msemo wa bible kuwa amani ya Mungu ipitayo uelewa woote......
vijana wanapiga miziki yamapenzi na kutogozana, wanaishia kuchanganyikiwa na kuuwana kama sio kubadili wachumba na kupata ukimwi
Je Unafurahi kwa kusoma hap?
ukijani huuu
Thursday, June 4, 2009
sara na maombi, je wewe unaombaga?

Sijui cha kupost nini maana nimebanwa na shughuli za kidunia vya kutosha sana. Japo tunasubilia majibu ya yasinta juu ya incarnation. Tuna kiporo cha meditation lakini duh, mambo magumu.\
Labda tuongelee juu ya sala. Eti sala au maombi ninini? Kwa nini watu huomba? Tofauti kati ya prayer / praying ndo ipi? Je unaamini juu ya nguvu ya maombi kwamba yaweza kuamisha milima? Kama ndio, wewe uliwahi kuombea nini kisicho cha kawaida na kikawa? Je ni kwanini sala au maombi ya wengi huwa hayafiki au hayajibiwi? Lakini ni kweli kuwa hayajibiwi?
Kwani wewe huwa unasali au kuomba? Je inabidi tusalie na kuombea wapi na wakati gani kwa kuelekea wapi? Kwanini kuna wanaoomba vijisanamu kama wakatoliki vile?
Jibu kadri ya majibu uliyonayo
Monday, June 1, 2009
Tuangalie juu ya re-incarnation
Maumbile (Mungu?) yaliumba mara moja. Ni siku ya uumbaji pekee ndipo kila kitu kilipoumbwa. Hakuna kazi nyingine ya kuumba iliyofanyika baadaye kama unaamini katika uumbaji kwani hata vitabu vitakatifu vinatwambia hilo.
Basi bwana, mimi nimekuwa nikiamini juu ya hilo na ninaamini kuwa niliwahi kuishi sehemu fulani kabla ya kuzaliwa tena leo nikiwa mhaya wa bukoba. Nimekuwa nikihoji watu wengi juu ya hili, wengi ukiri kuwa walipokuwa wadogo waliwahi kufikiria juu ya watu kuzaliwa pahala na kuzaliwa tena. Yanakumbukwa udogoni labda kutokana na kuwa na kumbukumbu ya tulipotoka.
Semina ya utambuzi pale FAJI, mwanafunzi mmoja alifundishwa meditation na hypnosis, kesho yake alitwambia kuwa alifanya hivyo akarudi nyuma na kuwaona wazazi wake wakifanya ile ngono iliyomleta yeye duniani! Hii inadhihirisha kuwa sisi ni zaidi ya miili na hatuna mahala pamoja.
Ilitokea nchini India, mtoto wa miaka kama 15 akafariki kwa ajali ya baiskieli na baadaye akazaliwa mtoto katika familia ya jirani, ajabu mtoto huyo alianza kuongelea juu ya ajali hiyo na alivyokufa! Mtoto huyo alianza kudai hata nguo zake za zamani kwani walizivaa wale waliokuwa wadogo zake kabla hajafa. Alisema jina lake alilotumia nk, nk.
Sasa katika TV show moja ya Oprah mmalekani, alionyesha dakatri mmoja nchini humo akiwa-hypnotize watu na kuwafanyia regression mmoja aliongea kichina, alipoletwa mkalimani, akasema huyu jamaa anajiona akiwa china sijui na watu gani hivi. Mwingine ni mwanamama naye ni mmarekani, alianza kuonge lugha ya majamaa wa Nepal, akaletwa makalimani.
Mama yule alijiona akiwa nchini Nepal kijiji fulani akiuza gengeni kwenye soko moja. Ili kujua kama ni kweli, wakasafiri kwenda Nepal. Wakauwauliza wenyeji wa mji ule juu ya uwezekano wa kuwepo soko na kila kitu. Wakapelekwa kwa mbabu mmoja. Mbabu yule alikubali kuwa enzi zili lilikuwepo soko na mambo kadhaa aliyoyasema yule mama.
Na Mzungu mwingine alienda nchini Mali, alipofika eneo fualani akahisi kama anapafahamu vile kama ndo kwao vile NK. Je wewe unaamini katika re-incarnation? Kumbuka sisi ni zaidi ya mwili na hivyo ni kweli kuwa tulikuwepo, tupo na tutakuwepo. Sio swala la imani bali la kisayansi. Kama unataka kujua uliishi vipi na wapi kabla ya kuishi kwenye mwili wako wa sasa, nendo kwa ma-hypnotist au tuwasiliane na kupeana tekiniki za hypnosisi. Sio imani bali ni ukweli na ni uhalisia.
Hiyo ndiyo proof kwamba binadamu wote ni kitu kimoja na sisi sote ni wa moja. Hata mitume kama Kristo ukisoma utagundua kuwa aliwahi kuishi kama watu fulani na baada ya kufa, nguvu yake ikaingia kwa petro na baadaye kwa Paul au Sauli. Mpaka sasa yupo ila hatumwoni kwa sababu tunamtafuta kwa macho, kiburi na ujuaji, ukitulia utamwona.
Je wewe utakufa au unataka kufa au kuishi milele?
Thursday, May 28, 2009
mbibi akisubilia mambo


mnamuona alivyompole, kuna jamaa kavaa 'vyeupe' anataka kumkabidhi kachakula fulani ka baada ya kipaimara. sasa nami naingia msituni ili nikue kiroho usiponiona hapa siku mbili tatu ujue sijakususa niko msituni, hija, polini natafuta kukua zaidi na zaidi au sio?
nakumbuka enzi hizo wanakuja kwetu kumlisha bibi kamkate hako, duh nilidhani kanatokea mbinguni
Tuesday, May 26, 2009
Nyegerage waitu! Amana vijana senta, byalimana
Utaratibu wa kunyoa nimeutelekeza kwa Muda. Kila nikienda saluni mashine zinawasha na muda unabana lakini pia nimeachana na mashindano ya kunyoa leo kesho zinaota. Kwa hiyo Markus aliona kama naelekeana na picha kwenye blog lakini akakaa kimya. Nilipomwambia kuwa ndiye Mimi mwenyewe, basi alishutuka, alifurahi na kunikumbatia. Tuliongea kwa Muda mfupi na akahaidi kukwambia na wewe kuwa tumeonana.
Mpangala aliniuliza, lilli neno Nyegerage linamaana gani? Nikajua ameshawaza sauzi Africa ya nguoni!. Basi nikafikiri na wewe una hofu na neno hili si unajua linafanana na yale ya kuamsha waliolala? Basi leo mambo yanabwagwa hadharani.
Neno Nyegerage linatokana na neno la Kihaya a.k.a kikwetu, Nyegera, Lenye maana ya karibu na nyegerage ni karibuni sana, huwa wanasema nyegerage mugile akanyeto wakimaanisha njoo kwa kwa madaha mmeshafika, karibuni. Hiyo ndiyo maana yenyewe.
Basi bwana, ukiwa maeneo ya Ilala to Buguruni, kuna kituo kinaitwa AMANA. Duh! Ili neno amana kule kwetu ukilitamka wanakushangaa kwani halitamkwigi hadharani. Kwetu ukisema amana ni kuongelea pale njiani ulipopitia kuingilia duniani a.k.a kuzaliwa. Basi usimwambie mhaya ashuke amana, atakuchapa makofi na kukushitaki, atakuuliza; wangambila nshuke amana? Olifakubi iwe kyana!
Basi bwana neno amana halitamkwi bukoba (buhaya) kwani ni tusi a.k.a siri wakati Rwanda wana neno Imana, neno hila hufanana lile la kihaya la kituo cha basi Amana japo kwao ndo jina la Mungu. Wanyaranda huita majina ya Byalimana wakimaanisha yote kwa Mungu lakini jina hili likitamkwa, wahaya huinama na kucheka kinoma eti kwao linamaanisha vimekula ile njia ielekeayo duniani kutoka mimbani! Duh basi kama wewe unaitwa byalimana, ukitambulishwa kule Bukoba, utaona majamaa yanakukaribisha kwa furaha na vicheko, usidhana yanakufurahia, yanakucheka ile mbaaaya kwa chakula hicho.
Hiyo ndiyo maana ya neno Nyegerage, karibuni sana. Kikwenu inamaana gani?
Monday, May 25, 2009
Tahajudi na wengine huita taamuli basi sisi tuiite meditation.
mdada kama huyu waweza dhanimkosawa kumbe labda ashapasua hanga yuko kama mbingu ya nane hivi kwa mjuao spiritual planesSwali hili lina maana kuwa amani ya kweli imo ndani mwako na hakuna awezaye kukupa wala kukunyanganya amani hiyo japo wengi hatuna na tunaitafuta kwa wenzetu na kamwe hatutaipata Utulivu wa akili kwa kiingereza wanasema ni peace of mind ndio utuletea amani ya roho na nyinginezo.
Kwa njia ya tahajudi na meditation utapata amani. Inasemekana nusu ya wakazi wa Dar ni nusu-vichaa kwa sababu ya kutokutulia wala kupata muda wa kulala vya kutosha. Wengi hushinda barbarani, kwenye daladala na ukiwa nyumbani kamwe huna utulivu. Usiposikia kelele za majirani basi utasikia mtoto akilia au gari likipiga honi au kelele za mwizi angalau jirani yako kafungulia redio hiyoooooo.
Ukifuatailia kwa miaka kadhaa wewe mkazi wa Bongo hujawahi kuwa Kimya bali unashinda kwenye kelele na hivyo huwezi kuisikia asili ikikuliwaza. (nature au Mungu)
Ni lazima tuwe na utaratibu wa kukaa mahali patulivu na kujiambia maneno yenye furaha naya kututia amani. Kwa mfano waweza kuandaa neno au kikundi cha maneno wengine huita mantra na kukirudia rudia. Kwa mfano; Amani, upendo mafanikio. Kaa mahali penye ukimya peke yako pasipo kuongea na mtu, fumba macho au angalia upande mmoja tu kama vile pembe, picha, kiti, nk.
Kaa zaidi ya muda wa nusu saa na ukiweza masaa ukirudia maneno hayo bila kusikiliza kelele za nje au kufikiria kitu kingine. Baada ya muda ukimaliza utajisikia amani, furaha na upendo wa kutosha. Ni vyema kufanya hivi kabla ya kulala na baada ya kuamuka kabla ya kuondoka kitandani.
Kaa jiambie unataka siku yako ienende vipi au kaa kumbuka yoote uliyoyafanya siku nzima kabla ya kulala na kujisifia kuwa umeweza kuyafanya yale uliyoyafanya kisha lala. Utapata amani ya kutosha nakwambia. Ni vyema kufanya meditation kwa masaa zaidi ya mawili lakini kwa kuanza, anza na nusu saa tu.
ONYO!!! Usiinuke haraka baada ya meditation. Kaa kidogo kama dakika tano kwani kuinuka ghafra sio vyema sana.
Kama wewe ni mtu wa dini basi waweza kuunda maneno au mantra inayoendana na dini yako lakini chunga kujiambia yale usiyoyapenda au mabaya. Kwa mfano usijiambie au kumwambia Mungu wako ulivyokuwa mtenda dhambi,no! kwani utazitenda kweli. Jiambie meneno kama, Yesu nakupenda, au nataka nimwone Yesu au Yesu kimbilio
langu au Mungu ni mkubwa.
Kwa waisilamu tumia kama ile ya ALLAH AKBAR nk.
Rudia rudi maneno haya kwa Muda mrefu na kwa utulivu. Huu sio muujiza kwani utaoona matokeo yake kila umalizapo kuyasema, utaondoa kelele kichwani mwako na kuwa na amani. Kichwa chako kina kelele ndio maana hata ukiwa peke yako utulii. Utasoma gazeti, utafugulia redio, utaenda kijiweni kuongea na washikaji au utamkaribisha mgeni lakini ukiwa na utulivu yote sawa.
Meditation ijaribu sio imani wala kusubili kufurahi baada ya kifo, ni uhalisia
Ifuatayo tutaona juu ya kuvuta vitu vizuri kwa njia ya meditation.
.
Sunday, May 24, 2009
kchimba dawa nako
ujumbe wa jumapili tundugumpendwa
Thursday, May 21, 2009
kwa nini wakristo hujiita wana wa ISRAEL?
kwa maana hiyo kumbe na wewe unaweza kuwa mu-Israel na usichangaye kutembea katika sheria ya Mungu na hofu juu ya Mungu kwani kumbuka Mungu ni upendo na sio vitisho vya kuogopwa. basi ndiyo maana wakristo huongela mbingu mpya na nchi mpya (yerusalemu mpya) sio mashariki ya kati plz. mbingu mpya ni pale utakapo mgundua Mungu wa ndani yako esp. kwa njia ya tahajudi (meditation) na kupata 'connection' na kuishi ukiwa connected na ile mbingu mpya (ndani mwako) ikitoka nje yako basi hiyo ndiyo nchi mpya (yerusalemu mpya) mwisho wa dunia ni pale tutakapo pata na kuishi katika uwepo wa Mungu (devine connectio) ambapo mwili wa akili (mind) utashindwa na kutawaliwa na mwili wa roho.
hapo hakutakuwepo na jambo baya wala zuri. kila jambo litakuwa ni jema kama biblia inavyosema kuwa alipomaliza kuumba, Mungu alsema yoooote ni mema japo mwanadamu akataka kujua mabaya kwa kula mti wa uelewa, akayajua mabaya mpaka leo yanampeleka puta. zambi tano za kifo ndo zinatawala; tamaa, hasira/visasi, ujuaji/ubinafsi, attachment, uchoyo na matatizo ya kiaiba (ego) mwisho wa dunia undugu, utaifa, ubaguzi wa rangi, mataba nk vitaisha kwani binadamu ataona ukweli kuwa woote tu wamoja tukiunganishwa na Mungu na Mungu ni mmoja na sote ni ndugu.
ndipo tutakapothamini viumbe na kuwa kitu kimoja, tutaishi kwa kumtukuza Mungu, tutaimba, tutasifu, tutawapenda wenzetu. ujinga wa kutengeneza siraha utaisha tutaingia kwenye ukweli halisi nayo hiyo kweli itatuweka huru. waubiri wenye kuombea watu wapate wake/waume, utajiri, vyeo nk watapukutika na tutakuwa na lengo la kumtukuza Mungu. upendo utaongezeka, amani ndo basi nk. hiyo ndiyo Yerusalemu mpya, mwili wako utakapotumika kama hekalu la Mungu badala ya kuwa karakana la kutoa mawazo, maneno na matendo mabaya.
yerusalemu mpya sio ile wanayopigwa wapalestina ili ijengwa, bali ni ile utakapofika mbingu mpya moyoni mwako na mbingu hiyo ikijidhiirisha kwa nje, basi hiyo ndiyo nchi mpya, itakuwa raha mustarehe, raha kuliko zile uziitazo raha. sihubiri wandugu, najaribu tu kuelezea maaana ya jina Israel na kuwa taifa teule la MUNGU aka NGUVU KUU aka SUPREME BEING aka UNMOVABLE MOVER aka THE ONE nk nk nk.
je unatamani kwenda yerusalemu wewe?
Wednesday, May 20, 2009
Fascinating Rwanda
Rwanda is a beautiful country. Infrastructure has been improved significantly for the past 15 years. You cannot imagine that it was in massive massacres before. Love is a predominant feature you will find among Rwandans.
Among ”fascinating” things I have discovered in some Rwandans, probably peculiar in the world are:
People can request a lift on commercial public transport and accepted, like city buses. When you hire a taxi, don’t be surprised people to come to your taxi driver and ask a lift while you are ignored, and of course a driver will offer them a lift without your permission despite that you will be the one paying (it happened to me more than once).
Some bank clerk can spend more than 30 minutes attending one client with simple transactions which at home hardly takes 5 minutes, and yet other clients don’t complain, but I was told that according to Rwandan traditional values “it is bad to complain”!!!
If you meet somebody whether you know him/her or you don’t, the greetings has to be by handshake, if you don’t, it signify hatred, and if someone you know him/her very well, then you must hague and gives each other three kisses on cheeks. Don’t be surprised if your way is blocked by friends when they meet along the road and greet each other, just pray they will not be more than 5, as all have to be treated the same way. Aye, greetings can take even 5 minutes or more if the group is big, even in the middle of supermarket, just find your way outer there otherwise......
Now, there are several workshop conducted to different firms especially those dealing with customers to improve hospitality and customer care.
Monday, May 18, 2009
wakazi wa Dar wanaisha kwenye magari na vituoni!
nikiongea na jaamaa yangu aishiye mbezi bich na kufanya kazi posta, aliniambia
kuwa kila siku huamka saa kumi asubuhi na kupanda basi saa kumi namoja na nusu asubuhi. hufika posta saa mbili kasoro. basi jamaa huyo hutoka kazini na kupanda gari saa kumi na moja na kufika saambili na nusu au tatu nyumbani!! ukipiga hesabu jumla, jamaa huyu anakaa kwenye dala dala zaidi ya masaa sita kila siku!!
duh, unashangaa! ama wewe ni mwanafunzi ndo maweeeeeee. saa kumi namoja upo kituoni daladala zinakuepuka kama mafua ya nguruwe. unakaa masaa lukuki na ukipanda ndo foleni kurudi hivyo hivyo! DUH
basi bwana, stori sio nyingi, kwa foleni za dar, watanzaniawaishio dar tunaishi kwenye dala dala na wengine kulala kwenye magari binafsi, kuna haja ya kujenga, kupanda na kununu nyumba nzuri wakati wanaishi ma-hausi gelo tu?
ndio maana washikaji wanaotamani kuhamia dar huwa nawashangaa na nashidwa kuwashauri, japo mimi naonekana bonge la chiiiizi kupanga kuhama dar! mh, niishi kwenye dala dala tena kwa kushika bomba au kwenye gari binafsi? duh.
Saturday, May 16, 2009
vijana wana umhuhimu gani katika mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa?
basi nipatieni japo yako maoni juu ya nafasi/umhuhimu wa vijan katika mabadiliko ya kijamii-kisiasa na kiuchumi "the role of the youth in socio-political and economic transformation".
nataka iwe pepa itakayobadilisha watu, vijana na sera za mataifa ya africa na kwa hiyo ni kazi kubwa naomba maoni yako. nitaiwasilisha pale IFM kwa njia ya video conference mwezi ujao na wewe nitakualika rasmi tuwe wote. ni mkutano utakaounganisha matifa zaidi ya saba ya kiafrika ikiwemo Tanzania, Uganda, Ghana, Ethiopian, Kenya, Madagascar, Zimbabwe, na afrika ya kusini
naomba maoni yako bwana si unajua tenaaaaaaa
Thursday, May 14, 2009
Wednesday, May 13, 2009
Tuesday, May 12, 2009
kuchapa viboko, moja na moja ni moja,
Kamala, nilichapwa hizo fimbo nikingali mdogo (nyumbani) na zilizidi nilipoingia shule hadi darasa la sita!
Leo hii nakubaliana nawe kuwa hiyo tandikwa tandikwa sio njia ya kufundisha watoto wetu. Na hata kwa wafungwa nayo haisaidii!
Nimevutwa na hilo la mantiki ya hesabu (moja ongeza moja ni moja).
Mantiki hii nimeitumia katika makala moja, niliyokwisha andika...lakini bado kuchapishwa... kuhusu demokrasia yetu nchini.
Hususan, nimeitumia katika mkitadha wa kujaribu kusuluhisha au kutafuta muafaka miongoni mwa sehemu za Muungano (Tanzania Bara na Tanzania Visiwa)...Napenda kuiita Tanzania Visiwa na wala si Visiwani, kama vile tunavyoiita Tanzania Bara na wala si Tanzania Barani!
Kwahiyo, niruhusu niiendeleze hesabu hiyo, ki-siasa:
Akingali hai, Mwenyekiti wa CCM Mwalimu Julius Nyerere alilikemea kwa ukali pendekezo la kuunda federesheni na serikali zake tatu, yaani, Serikali ya Tanzania Bara, Serikali ya Tanzania Visiwa na Serikali ya Muungano.
Mwalimu Nyerere alidhihirisha kwa mantiki yake kwa hesabu za vitu-guswa (au vitu-onekana).
Ni hesabu ya mwanzo kabisa: moja ongeza moja ni mbili. Nyerere alikataa kata ya kukubali: moja ongeza moja ni tatu!
Mpaka sasa tunaamini kuwa jumla hiyo ya moja ongeza moja ni mbili ni kweli kila mara bila kujali mikitadha! Ndio maana hata Mwalimu Nyerere alikazania kuwepo kwa serikali mbili tu.
Mimi binafsi si mtaalamu wa hesabu – somo lililokuwa likinipa ushindi wa chini shuleni.
Naafiki na Mwalimu Nyerere kwa dhati kwamba katika mikitadha ya hesabu/nambari za vitu-guswa au vitu-onekana viwili: moja ongeza moja ni mbili.
Lakini si kweli hata kidogo katika mikitadha mingine!
Kwahiyo, ninahitilafiana na Mwalimu Nyerere kwa kufikiria kuwa Tanganyika na Zanzibar ni vitu-guswa au vitu-onekana!
Tanganyika na Zanzibar sio chungwa au embe, ambayo chungwa moja ongeza chungwa moja ni machungwa mawili ua embe moja ongeza embe moja ni maembe mawili!
Tanganyika na Zanzibar ni ideas. Na mantiki yake ni ya moja ongeza moja ni moja!
Na hii iko sawa pia kwa vitu-onekana vyenye uwezekano wa kuunganishwa, kwa mfano, majumba. Majumba mawili yakiunganishwa, linakuwa ni jumba moja tu kubwa).
Nitatoa mifano miwili kudhihirisha mantiki hii ya moja ongeza moja ni moja kutoka katika Biblia. Mifano hii ni kati ya vitovu vya imani ya wa-Kristu:
Mfano 1: Mwanzo 2:24 na Marko 10:7 tunaambiwa kuwa mwanaume na mwanamke wakioana wanatekeleza idea ya ndoa inayovuka mikitadha ya vitu-guswa au vitu-onekana viwili (mwanaume na mwanamke)!
Cha maana kinakuwa ni ndoa; ni mkataba. Na mkataba wa ndoa, kama ilivyo mkataba wowote, hauvunjwi hovyo hovyo! Wawili hao wanafikiriwa kuwa kitu kimoja.
Kwahiyo, tunaweza kutamati kuwa ndoa ya ki-Biblia inauminisha kuwa moja ongeza moja ni moja!
Kwa waliooana, kama kila mmoja atajiona kwamba moja ongeza moja ni mbili, basi mtafaruki utaanza na kuleteleza kutengana, kuachana na kuvunjika kabisa kwa ndoa yenyewe, hatimaye.
Matokeo yake yatakuwa kwa hao wawili kubakia ya moja ongeza moja ni mbili!
Mfano 2: Kwa kifupi, imani ya ki-Biblia inawaasa waumini kuwa kuna Mungu mmoja tu ingawa kuna Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu (Utatu Mtakatifu).
Kwahiyo, mfano huu ni sawa na kusema moja ongeza moja, ongeza moja na ongeza moja ni moja na wala si tatu!
Tuingie ya kwetu hapa - ya ki-dunia - kwa kutoa mifano minne:
Mfano 1: Bila kujali ukubwa, eneo, uzito, ujazo, na kadhalika, tuangalie ya vimiminiko au dabwadabwa, kwa mifano, matone ya kahawa, lubisi, kangara, ulanzi, maji, maziwa, chai, asali au damu (hakuna cha ushirikina hapa), na kadhalika.
Ukidondosha tone moja la kahawa juu ya karatasi au chombo kingine, halafu uongeze tone la pili juu ya la kwanza, huwezi kuona matone mawili; utaona tone moja tu kubwa kwa vipimo vyake.
Na unaweza kuongeza tone la tatu au la nne huwezi kuona matone matatu au manne ya kahawa! Utaona tone moja tu kubwa kwa vipimo vyake!
Kwahiyo, kulingana na mkitadha huu, moja ongeza moja ni moja!
Mfano 2: Tuangalie mkitadha mwingine, u-rafiki.
Kama ilivyo ndoa niliyoitaja hapo juu, u-rafiki wa watu wawili (au zaidi) ni sawa na moja ongeza moja (hadi kufikia hiyo jumla ya nambari ya ma-rafiki) ni moja!
Kwahiyo, kiini cha u-rafiki ni moja!
Mfano 3: Tuangalie tena ya mikoa ya nchi yetu. Kama mikoa miwili ya Lindi na Mtwara ikiungana, itakuwa ni moja ongeza moja ni moja (mkoa mmoja mkubwa kwa vipimo vyake)!
Mfano 4: Tuangalie ya timu ya mpira wa futiboli (soka) au kandanda. Upande mmoja huchezwa na watu 11. Lakini hatusemi tumeingiza uwanjani wachezaji wetu 11; tunasema tumeingiza uwanjani timu moja.
Kwa mantiki hii hii, ili kuendeleza Muungano wetu wa nchi mbili huru za Tanganyika na Zanzibar zilizoamua kuungana (wa-Uingereza wanaita, to exercise a political marriage of convenience), tuuchukulie Muungano wetu kwa mifano ya ndoa, Utatu Mtakatifu, urafiki, jumba, mikoa, timu au matone mawili ya kahawa, lubisi, kangara, ulanzi, damu, maji, asali au soda bila kujali ukubwa au udogo wa kila tone!
Tukizingatia saizi, kwa mantiki hii hii, tone moja kubwa (Tanganyika) ongeza tone moja dogo (Zanzibar) ni tone moja kubwa zaidi (Tanzania)!
Mantiki hii inaweza kabisa kutusaidia kunasua a political marriage of inconvenience inayojining’iniza machoni petu, kuhusu Muungano wetu!
BAP
Sunday, May 10, 2009
nina machungwa matanosio manne; moja + moja ni ni moja
watoto kama hawa unyeshewa mvua ya viboko kwa sababu ya busara zao wazitoazo mbele ya ajinga (wazazi, walimu,walezi na wewe)aisee wengi mumelelewa katika mazingira ya kuchapwa viboko na waliojuu yenu. siku zote napinga kuwachapa wanetu na wadogo zetu kwani sipendi wajisikie kama mimi nilivyojisikia nilipochapwa. naamini katika ukaribu, kubebeana, kusameheana na kujadiliana.
basi inasemekana Kim JongHill aliulizwa moja kujumlisha moja ni ngapi? akajibu ni moja. ungekuwa wewe shule za kjijini kwenu basi ungemwagiwa mvua ya fimbo na matusi jinsi ulivyokuwa zoba, japo yawzekana akwambiaye hivyo ni zoba zaidi yako.
basi bwana Kim aliambiwa adhibitishe jibu lake, akasema; nikiwa namwagia maji bustani, viudongo viwili huruka na kutua juu ya jani, viundongo hivyo utengeneza kiudongo kimoja kikubwa zaidi na kwa hiyo moja kujumlisha moja ni moja na sio mbili! kuna mantiki hapo ungekuwa wewe mamaaaaaaaaa pwaaaaaaa mpaka ngozi ibanduke!
basi mwalimu mwingine alimpatia mwanafunzi machungwa manne, akamuuliza una machungwa mangaipi? dogo akasema matano. basi mwalimu akamnyanganya na kumpatia mawili, kisha mawili na kumuulza una machungwa mangapi? dogo akasema matano! duh!
yule ticha akapagawa,akamtukana kidogo kisha akamnyanganya machungwa yote na kumuuliza tena, sasa una machungwa mangapi? dogo akajibu moja! duh, ticha akaona dogo lilivyokuwa zoba, akaagiza fimbo, wakati fimbo inafuatwa, ticha akauliza liko wapi hilo? dogo akasema liko nyumbani alipewa na baba asubuhi!!!!!!
kumbe ticha ndo zoba. kwa hiyo huwa tunatumia viboko kuingiza ujinga vichwani mwa tuwachapao badala ya kujifuza busara zao!!!
wewe je!? usipigane namtu wala mtoto. yawezekana ana akili kuliko za kwakowewe.
eti we ni zoba mbele za mwanao ehe??
Friday, May 8, 2009
We mtoto utalaaniwa, maweeeeeee
Nilikataa kumtembelea na kumjulia khali kiongozi mmoja wa dini, nikakumbushwa kua yeye ndiye mtoa laana na baraka na hivyo anaweza kunifanya zoba na kuniamria kwenda kwa kaka shetani \9kama kweli yupo)
Nikajulishwa juu ya stairi ya maisha yangu kuwa nisipokuwa makini na kufuata ninayoambiwa na wazee, basi nitaalaaniwa na kufia mbali au kuwa zoba!
Duh! Nilienda kumtembelea mchungaji Fulani, nikambishia na kukataa mikwara yake, akanishitaki nikaonywa juu ya laana!
Kila ubishi wangu au mtizamo wangu, ni wa kudai laana tu. Yaani mimi siwezi kuwa na maoni au mitizamo kwani kufanya hivyo nitalaaniwa!
Aisee yaani kila maongezi ni lazima nipigwe mkwara wa laana. Ila niligundua wazee wanatumia msemo huu ili kulinda hatma yao kwani uzee umeingia na hivyo wanahitaji ukaribu na vijana kwa hiyo wanajilinda kwa kukumbusha juu ya uwepo wa laana bila kukumbuka kuwa dua la kuku halimpatagi mwewe siku zote kwani anapaa na kuruka dua hilo
Siamini juu ya uwepo wa laana hata kidogo. Lakini nilijiuliz swali ,je kwani mimi sina laana? Nikimaanisha; mimi siwezi kuwawahi na kuwalaani wale woote wajifanyao wana uwezo wa kunilaani?
Mtu akinipiga mkwara wa kunilaaani, namtangulia na kumwahi kwani na mimi laana ninayo na haina umri na labda yangu nikali kuliko yake!
Thursday, May 7, 2009
kinyawawa, ekinyawawa au ebinyawawa

fu shambani mwako au karibu na kwenu ndo maweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee ukimkuta kafa njiani wewe geuza njia urudi kwako. ukimsikia analia usigeuka asije akakutwanga mkosi wa kifo! duh naishia hapa
Tuesday, May 5, 2009
Munga tehenan; kifo chake sasa ni mwaka M1
nilikwenda kumjulia hali, nikamkuta anapumua kwa mashine, kwa ugumu wa kuongea, akaniangalia na kusema, 'kamala, karibu, hali yangu inaendelea vizuri, kama nisingeletwa hapa (hosp) jana, sasa hivi mngekuwa mnajiuliza huu mwili muutupe wapi, kama ni Moshi, Morogoro au Dar'
alipojaribu kunielekeza kitu, wakaingia madaktari na kuniamuru niwapishe kidogo, na walipoondoka alikuwa amezuiwa kuongea tena na kucheka kwani vilimaliza nguvu. aliongea kwa ishara tu kila nilipomtembelea. ilikuwa ni siku ya jumapili tarehe nne, nikiwa naishi eneo la posta, nilifika Hindu mandal kumjulia khali, nilizuiwa kuingia kwani muda ulienda sana. jumatatu ya terehe tano, nikiwa naelekea hospitalini hapo, ilingia SMS kwenye kiselula changu kuwa, Munga amefariki asubuhi hii!
nikastuka, lakini nikakumbuka jinsi Munga mwenyewe alivyonifiundisha kutokuogopa wala kutishiwa na kifo kwani nikizuri. nilifika hospitalini mida ya saambili asubuhi na kumkuta mwanafuzi mwenzangu Aisha, akiwa amesimama machozi yanamlengalenga. nilichungulia dirishani, mwili wake ulilazwa na kufungwa kama gunia la viazi, basi nikasaidia kuupeleka mochwari, keshoyake tukauzika mwili ule kwenye makaburi ya kisutu hapa jijini.
kifo cha jamaa huyu alikijua mapema kwani alikuwa akituaga darasani nasi tusijue anamaanisha nini. changamoto ikabakia kwetu kueneza alichotufundisha na sisi kuendelea kuwa imara. mpaka sasa tunaendelea kujifunza utambuzi, kujitambua na kuwaelimisha wengine kwa njia ya ana kwaana na mtandaoni. bado tunachangamoto ya kurudisha gazeti la jitambue sokoni.
namshukuru Munga kwani alinibadilisha haswa, maisha yangu yakawa yamaana na kuondoa vurugu, maumivu na matatizo ya kihaiba (ego). japokuwa hakuwa muumini wa dini yoyote, mwili wake ulizikwa kwa taratibu na 'heshima' zote za dini ya kiisilamu aliyokuwa amezaliwa na kulazimishwa kuifuata kama wengi mfuatavyo dini mlizochaguliwa na kulazimishwa kuzifuata.
aliacha mke, watoto wa 3; Kilonzo, Nuru tatu na mwingine. kituo chetu alichokianzisha kinaendelea vizuri pale kimara-Rombo.
sasa anafurahia maisha nje ya mwili kwani alionekana kuchoshwa sana namaisha ya mwili na kabla ya kufa aliandika makala tatu za kutuaga ikiwemo ile ya tutaogopa kufa mpaka lini, maiti hii ni ya nani nk.
je wewe ukifa utaacha nini cha kubadilisha jamii?
Monday, May 4, 2009
Hii ndiyo dini yangu -- hitimisho

Katika post ya kwanza juu ya dini yangu ndg fred katawa alitamka dini kadhaa kuwa ndiyo zangu. Nilishangaa na kujaribu kukubaliana naye. Misahafu karibia yoote huongelea kitu kimoja na kitu hicho pia hukiongea kwa lugha na tamaduni tofauti japo ukifuatilia kiini basi huwa kimoja.
Kinachowachanganya binadamu wa sasa wenye kutaka ugomvi huwa ni lugha tu na mazingira kitu hicho kilivyosemwa.
Dini zote huamini katika utu, umoja, ushirikiano na mshikamano. Zote huamini katika Nuru (mwanga), sauti (neno) na upendo. Huwezi kumtofautisha Mungu na upendo na huwezi kumtofautisha mwanadamu na upendo. Kwa hiyio Mungu na mwanadamu na mwanadamu na mwanadamu huunganishwa na upendo na hivyo upendo ndio msingi wa misahafu yote.
Dini nyingi huamini wasichoelekezwa na waasisi wake na hivyo hufuta maagizo ya wanadamu. Wakatoliki hupenda kujigamba walivyo kuwa kanisa kubwa duniani lenye waumini wengi japo waumini hao na ukubwa wa kwanisa hilo havinamaana sana kwani bado yale maasi yanayopingwa na dini hiyo yanazidi kuongezeka kama waumini waongezekavyo.
Mengine huwakumba mpaka viongozi wa dini zenyewe.
Kwahiyo sio vyema kujivunia ufuasi wako badala yake muhimu ni kufuata maelekezo ya dini yako na kukua kiroho zaidi. Tunaenda mbinguni tukiwa hapahapa kwanzana lengo letu liwe na kuifanya dunia kuwa paradizo na sio vinginevyo.
Basi huwa napenda kusalia katika kila dini. Msikitini huwa siendi ila nasikilizaga tu mihadhara yao kwani mike zake ni pana (vipaza sauti). Nikiwa Dar, mara moja kwa mwezi, huwa naenda KKKT-azania, au DPC kinaondoni kubadilishana mawazo na kuonana na washikaji na kufurahi kidogo juu ya vitisho vya kuingia motoni usipotoa sadaka ya kutosha!
Katikati ya wiki nikiwa na muda basi huwa naingia kwenye kijikanisa kidogo cha mtakatifu Yosefu ili kupata meditation moment. Binfasi naamini katika Nuru, sauti, Upendo. (Love and respect to every God’s creation)
Imani yangu inanifanya kutokuwala wenzangu na hivyo kuwa vegetarian! Siamini hata kidogo bali natenda. Wabadha wanaita ‘ihi passika’ njoo uone na sio uamini tu! Kwa hiyo najua na nikishajua natenda na nikishatenda naona na kuzidi kujua—ndiyo sara yangu.
Siombi kimyakimya na kusubili majibu kesho au kwenda mbinguni baada ya kufa. Natenda na kupata majibu pale pale kama ni mbinguni kufika sio ishu yaani, nikukaa na kutulia na kujiendea nakurudi!
Basi naamini katika kutokuwatendea wale ambaya mimi sipendi kutendewa. Kufanya kazi kwa bidii, kuwasaidia wengine nk. Fred alipatia kwani nasoma misahafu karibia yote niliyonayo na niikutayo maktaba na internet. Sisi tu wamoja bwana.
Kwa kifupi hiyo ndiyio imani yangu, iliyonifanya kuijua mbingu na nchi mpya, wakristo waiitayo Yerusalemu Mpya.
Niulize ni ipi hiyo?
Thursday, April 30, 2009
picha za home bwana
















