

ndg,
angalia hizo picha mbili, majamaa wanasaidiana kuruka ukuta ili wakaangalie mpira, harafu wakiisha kuwa ndani basi ni ubabe kwa kwenda mbele. sasa angalia hiyo picha ya chini mijamaa inapimana nguvu.
udogoni nilishabikia saana mpira. mpaka nakuwa kijana niliitwa Jonas Lunyamila (jina la mchezaji wa yanga) na baadaye nikaitwa davd becham kwa sababu nilicheza namba saba. nashangaa kwanini nilioewa majina wa wachezaji wakubwa namna hiyo wakati mpira ulikuwa haupandi! nilikuwa nikiingia uwanjani dakika za mwisho au kujaza tu pengo!
ningeweza kujifunga au kuacha mpira nikakimbia mbiyoooo kama vile nina mpira! duh, asikwambie mtu.
basi ukubwani nilipunguza hiyo hamu ya mpira. miaka yoote niliyokaa Dar sijawahi kuingia uwanja wa Taifa zaidi ya kupita kwa nje nielekeapo mbagara rangi tatu. kilichonikatisha tamaa ni baada ya kusikia story za kutisha kuhusu utazamaji.
eti ukikaa upande wa simba, yanga ikafunga ukashangilia, unatwangwa mkanda! mara majamaa wanakujoa kwenye chupa ya maji na kukurushia! duh mara nini. sasa angalia hao wanavyokamatana mashati
1 Maoni::
Ha ha haa, ustaarabu kwetu wabongo.., hatujui hata maana yake
Post a Comment